Skip to main content

Posts

Showing posts from January, 2016

Kilimo na Hifadhi Bora Ya Vitunguu Maji

Utangulizi Vitunguu ni zao muhimu sana hapa Tanzania. Mikoa ya Arusha, Manyara, Iringa, Mbeya, Tanga, Singida na Kilimanjaro ni maarufu sana kwa kilimo cha vitunguu na ni zao la chakula na biashara kwa mkulima mdogo. Uzalishaji wa vitunguu bado ni mdogo (tani nne kwa hekta) na upotevu wa mazao baada ya kuvuna ni mkubwa (50 %– 80%) kutokana na hifadhi duni hivyo wakulima  wanahitaji utaalamu wa kilimo bora na hifadhi ya vitunguu ili kuongeza uzalishaji na kipato. Uzalishaji wa vitunguu Zao la vitunguu linazalishwa kutokana na mbegu na miche inakuzwa kwenye kitalu kabla ya kupandikizawa shamban. Miche inakuwa na kuzaa vitunguu.Vitunguu vikikomaa, vinavunwa na kuhifadhiwa vikiwa katika hali ya kulala bwete. Katika hali hii vitunguu vinaweza kuhifadhiwa kwa muda mrefu aitha kwa ajili ya kuzalisha mbegu msimu unaofuata au kuuza. Wingi na ubora wa zao la vitunguu hutegemea; hali ya hewa, aina ya vitunguu, upatikanaji wa mbegu bora, kilimo bora, uangalifu wakati wa kuvuna, usafirishaji na hif

Ya kuzingatia Katika Kilimo cha Nyanya

Mbegu Pendelea kupanda mbegu za hybrid km ana eden nuru nk ilimradi iwe hybrid. Ardhi Ardhi iwe nzuri yenye rutuba kama haina rutuba weka samadi na pia tumia mbolea za kisasa. Dawa Ni muhimu sana kupulizia dawa mara kwa mara kuanzia kwenye kitalu cha mbegu hadi shambani. Mbolea Inapaswa kuweka mbolea mara mbili hadi tatu kulingana na rotuba ya shamba husika. Pia unatakiwa uweke vijiti ili kuwezesha miche kusimama vizuri na kuifanya isianguke nakuozesha matunda. Ukizingatia hayo utafanikiwa kwenye kilimo chako cha nyanya. Pia  zao la nyanya linaweza likakuongezea kipato na kakupa faida kubwa endapo tu utazingatia kanuni zake.

Kilimo

Kilimo ni uzalishaji wa mazao kwenye mashamaba. Kilimo kina maana pana inayojumuisha mifumo ya uzalishaji mimea, ufugaji wa wanyama, na uvuvi wa samaki. Mara nyingi kilimo cha mimea kinaenda sambamba na ufugaji wa wanyama. Watu hupanda mimea na kuitunza hadi mavuno hasa kwa uzalishaji wa chakula cha kibindadamu na lishe ya wanyama lakini pia kwa shabaha ya kupata malighafi mbalimbali zinazotumiwa kwa kutengeneza nguo za watu. Siku hizi kilimo kinalenga pia nishati ya mimea. Historia Watu walianza kulima takriban miaka 10,000 iliyopita na kabla ya hayo watu waliwinda tu na kukusanya matunda. Kuna vikundi vidogo ambavyo vinaendelea na maisha haya hadi leo lakini siku hizi zaidi ya asilimia 99 ya binadamu hupata chakula kutokana na kilimo. Inaaminiwa ya kwamba kilimo kilianza katika sehemu tatu za dunia ambako watu walitambua mimea yenye lishe kubwa na kupanda mbegu zao. Maeneo haya ambako kilimo kilianza ni China, Amerika ya Kaskazini na Mashariki ya Kati. Wataalamu hawakubaliani kama k