Skip to main content

Posts

Showing posts from February, 2016

Mchanganuo Kilimo cha Mananasi

Gharama Ununuzi wa ardhi kwa Tsh. 300,000--  Utayarishaji wa shamba Tsh 150,000/= kwa ekari - hatua 70x70 Gharama ya miche na upandaji miche 15,000 kwa ekari Tsh 750,000 (i.e.50 x 15,000 ikijumuisha ununuzi wa mbegu na upandaji), Mbolea 100,000. Matumizi mengine 200,000 (ikiwa ni pamoja ni vibarua, na kuleta mzigo sokoni). Jumla 1,500,000/- Mapato Nanasi unavuna baada ya miezi 18. kwa hesabu za chini kabisa unauza nanasi moja kwa Tsh 500 na assume unapata nanasi 12,000 utapata Tsh 6,000,000/=. (assumption ni kuwa si rahisi kupata mavuno 100%- bali inaweza kuwa 80%) Faida ukiondoa matumizi (Tsh 1,500,000) unapata faida 4,500,000 ukiwa na ekari tano bila shaka utapata zaidi ya milioni 20 (na hapo hujaweka economy of scale). --though unaweza kupunguza au kuongeza asilimia fulani kutegemeana na risks zilizopo na uzoefu wako katika kusimamia na kutafuta masoko.. Masoko  Soko lipo huko huko shamba au unaleta mjini mfano kwa BAKHRESA anayenunua matunda kwa ajili ya kutengeneza juice. Pia tuku

Maelezo ya Msingi Kuhusu Kilimo cha Mboga Mboga - Vegetables

Imetolewa na: Tushikamane Centre, Kilakala Road-Morogoro Mboga ni mmea au sehemu yoyote ya mmea inayoweza kuliwa na binadamu ambayo haina sukari kama matunda. Mboga huweza kuliwa zikiwa zimepikwa na mara nyingi huwekewa chumvi ili kuongeza ladha na pia huweza kuliwa zikiwa mbichi kwa mfano kwenye kachumbari. Mboga ni sehemu muhimu sana katika mlo uliokamilika, hii imesababisha ukuaji wa kasi wa soko la mboga na upandaji wa mboga katika maeneo mengi ya mijini na vijijini. Sehemu za mmea ambazo zinaweza kutumika kama mboga Majani Mboga nyingi hutoka kwenye majani ya mimea. Mara nyingi haya majani huwa ya rangi ya kijani kwasababu ya kutengeneza chakula cha mmea kutoka kwenye mionzi ya jua na huwa na virutubisho vingi muhimu katika mwili wa binadamu kwa vile vitamin. Miongoni mwa majani ambayo huliwa kama mboga ni Kabichi, Spinach, Chinese, Mchicha na figiri. Mizizi Mizizi ya baadhi ya mimea ni mboga nzuri na ina virutubisho kama vile vitamin A ambayo huimarisha macho na kuongeza uwezo wa