Skip to main content

Aina na Faida za kufuga Mbuzi


Utangulizi
Ufugaji wa mbuzi hapa ni fursa nadra ambayo Watanzania wengi hawajaiona. Ni ufugaji ambao wenyewe kama mfugaji atazingatia kanuni na misingi ya ufugaji Bora, ni rahisi sana mfugaji kujiondoa kutoka kwenye umasikini na kuwa tajiri. Kitu cha msingi na muhimu ni kwamba,mfugaji lazima awe na eneo pamoja na mtaji wa kuanzia.

Hawa ni mbuzi bora walioboreshwa, wanapatikana dodoma. Ni matokeo ya cross breed iliyofanyika kati ya mbuzi wa kienyeji wa dodoma na exotic breed.Hivyo wengi wa uzao wao huzaa mapacha. Mbuzi hawa huuzwa tsh elfu 50, wakiwa na umri wa miezi 5.

Sehemu ya kufugia
Mbuzi wanatakiwa kufugwa shambani. Shamba ambalo mbuzi wanatakiwa wafugwe linapaswa liwe na sehemu ambayo mbuzi wanaweza kwenda kuchungwa na pia kuwe na chanzo cha maji. Mbuzi kitabia hupenda kulala juu hivyo mabanda yao yanapojengwa lazima yainuliwe juu. Mabanda ya mbuzi si ghari,kwani hujengwa simple.

Uzaaji
Mbuzi kwa mwaka huzaa mara mbili na ukipata ile mbegu ya wanaozaa mapacha faida yake huwa ni kubwa zaidi, itategemea na mtaji wa mfugaji, lakini kama mfugaji ataweza kuanza na mradi wa mbuzi 50 inakuwa vizuri zaidi. 
Ukinunua mbuzi 50@ tsh.50,000/= utapata Milioni 2 na nusu [2,500,000], madume 2 kila moja likanunuliwa kwa tsh 75000/= kwa madume mawili itagharimu tsh laki moja na nusu. 
Usafirishaji wa mbuzi hauzidi laki tatu na nusu. Kwa hiyo utajikuta ukiwa na milion 5 utaweza kuanza na mradi wa ufugaji wa mbuzi majike 50 na madume mawili,pamoja na kuwajengea sehemu ya ya kulala.

Mbuzi kwa mwaka wao huzaa mara 2, hivyo kama kila mbuzi atazaa hebu chukulia kila mbuzi atazaa mbuzi mmoja tu, ingawa kuna wengine watazaa mapacha hasa ukipata ile mbegu ya mbuzi wanaozaa mapacha, mwishoni mwa mwaka utakuwa na idadi ya mbuzi 100 wapya waliozaliwa na ukujumlisha na mtaji ule wa mbuzi 50 utakuwa na jumla ya mbuzi 150, hii ni ndani ya mwaka mmoja, pata picha utakuwa na mbuzi Idadi gani baada ya miaka 3 hasa ukizingatia kuwa wale watoto wa mbuzi watakapofikia miezi 8 utaanza kuwapandisha nao watazaa nk. 

Magonjwa
Magonjwa ya mbuzi mengi yanafahamika na ni rahisi kudhibitika,hivyo mbuzi si rahisi kufa hovyo.
Toka mbuzi anapata mimba mpaka anazaa,hutumia muda wa miezi mitano yaani siku 150.

Ya kuzingatia
Ili kufikia malengo, inashauriwa kuwa mbuzi wa mtaji wanaonunuliwa lazima wawe na umri mmoja ili kusudi waweze kupata mimba kwa wakati mmoja na waweze kuzaa kwa wakati mmoja pia.



Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

Utengenezaji wa Chakula cha Kuku wa Nyama (Bloilers)

Utangulizi Kuku wa nyama wana mahitaji yafuatayo ya viinilishe katika chakula ili wakue vizuri Viinilisha vya wanga 60-65%   Protini 30-35%   Madini 2-8% Chakula cha Vifaranga Chakula hiki hutengenezwa katika namna ya kumsaidia kifaranga aweze kumeza vizuri na hivyo hakitakiwi kuwa katika punje punje. Hata kama utanunua pumba, ni vema kuzipitisha kwenye mashine ili ziwe laini zaidi.  Mahitaji (kgs)  Unga wa dona wa nafaka kama mahindi au mtama 40  Pumba za mtama au mahindi au uwele 27  Mashudu ya alizeti au ufuta, au pamba au karanga n.k. 20  Unga wa mifupa au chokaa ya kuku (DCP) 2.25  Dagaa au mabaki ya samaki (sangara fish meal) 10  Chumvi ya jikoni 0.5  Virutubisho (Broiler premix) 0.25  Jumla utapata 100Kg. Chakula cha kukuzia – growers mash Mahitaji (Kg) Mahindi yaliyobarazwa au mtama au uwele 25   Pumba za mtama au mahindi au uwele 44   Mashudu ya alizeti au ufuta, au pamba au karanga n.k. 17   Unga wa mifupa au chokaa ya kuku (DCP) 3.25   Dagaa au mabaki ya samaki (fish meal) 1

Aina Za Miti ya Minazi

AINA ZA MINAZI Inafaa mkulima kufahamu kuna aina mbali mbali za minazi na ina mahitaji tofauti katika ukuaji. Ujuzi huu utamsaidia katika kuchagua aina ya minazi itakayofaa kwa eneo lake na kwa kiwango chake cha utunzaji. KUNA AINA TATU ZA MINAZI Minazi mirefu ya asili Minazi mifupi Minazi chotara MINAZI MIREFU YA ASILI (EAT) Minazi ya aina hii ndiyo inayojulikana na wakulima wengi kwa vile ni ya kiasili na imezoea mazingira yetu. Minazi hii huchukua miaka 6-8 tangu kupandikizwa hadi kuzaa. Minazi ya aina hii huvumilia ukame na inao uwezo wa kutoa wastani wa nazi 40 kwa mwaka. Nazi huwa kubwa na zenye nyama nene ambayo inafaa kwa kupikia na kukamua mafuta. Minazi hii huishi kad ya miaka 60 na kuendelea. Nchini Tanzania, minazi hii hustawi vyema ukanda wa pwani sehemu zisizo na mawe na ambazo hazituamishi maji. MINAZI MIFUPI (DWARF) Minazi ya aina hii huzaa mapema kuanzia miaka miwili. Huzaa nazi nyingi na ndogo. Nazi hizi huwa na nyama nyembamba hivyo hutumika kwa nnadafu. Minazi huhit

Kilimo cha Miti ya Mbao - Uwekezaji wa Muda wa Kati na Mrefu

Utangulizi Kilimo cha miti ni uwekezaji wa muda wa kati na mrefu (mid & long term investments). Ila kwa kawaida jamii nyingi hasa za kiafrika huwa hazivutiwi na uwekezaji wa muda mrefu. Hata hivyo kama una mpango wa kuwa imara kiuchumi inashauriwaau yakupasa kufikiria na kujifunza aina za uwekezaji wa muda mrefu. Miti hutumika kwa matumizi mengi mfano mbao, nguzo za umeme na kujengea, mapambo, kuni na mkaa, kuzalisha matunda, mitishamba na madawa,  utengenezeaji wa karatasi n.k.  Mchanganuo Ekari moja ya shamba unaweza kupanda miti mia sita (500) mpaka mia saba (700). Gharama za kununua mashamba au maeneo ya kupandia miti hutegemea na eneo. Kwa  sehemu nyingi za vijijini maeneo kwa ekari moja hayazidi laki 5.  Miche ya kununua mfano Mitiki huuzwa kuanzia elfu moja (1000) kwa mche mmoja Gharama ya kununua miche =  1000 * 600 = 600,000   Pia unaweza kuokoa gharama za kununua miche kwa kuioteshe mwenyewe ktk vitalu na kuiamishia shambani baada ya kustawi vizuri na kuwa imara.  Mf. Mbe