Skip to main content

Chanjo ni Bora Kuliko Dawa - Umuhimu wa Chanjo kwa Kifugo


Utangulizi
Mifugo ni rasilimali ambayo huwapa faida kubwa wafugaji na wananchi kwa ujumla. Ili mifugo itoe mazao yenye tija inahitaji kupatiwa huduma bora za malisho, maji, kinga na tiba za maradhi. Maradhi ni moja kati ya matatatizo yanayozorotesha sekta ya ufugaji na kupunguza uzalishaji. Katika kukabiliana na changamoto hiyo hatua za kuyadhibiti maradhi zinachukuliwa duniani kote ili kuimarisha ufugaji na kupata tija.

Chanjo
Chanjo ni mchanganyiko maalum wenye vijidudu ambavyo vimepunguzwa nguvu ili visilete madhara kwa wanyama au watu waliochanjwa. Hii ni njia mojawapo inayotumika katika kudhibiti maradhi duniani. Asili ya chanjo ilitokana na ugunduzi wa mwanasayansi wa Uingereza Bw. Edward Jenner katika karne ya 18 ambapo aligundua kwamba wahudumu wa ng’ombe hawakupata ugonjwa aina ya ndui (small pox) kutokana na kuwa na vijidudu vya ugonjwa wa ndui za ng’ombe (cow pox) hali ya kuwa maeneo mengine wasiokuwa wahudumu wa ng’ombe waligundulika kuwa na ugonjwa huo.
Chanjo husababisha mwili wa mnyama au binadamu kuandaa askari (vikinga mwili ni antibody) ambao hukaa mwilini kwa muda maalum na huukinga mwili kukabiliana na vijidudu vya maradhi. Aidha, chanjo ikipungua nguvu inahitajika wanyama wachanjwe tena kwa muda maalum uliopendekezwa kutokana na aina ya chanjo au mnyama.

Aina za chanjo
Miongoni mwa chanjo maarufu zinazotumika kwa mifugo ni; Hitcher B1, LaSota, S19/ Rev- 1 strain, Blanthrax, Rabisin, Tetanus Toxoid, Newcastle Disease vaccine EDS – 76 + ND + IBD, Fowl pox, Clon CL/76 strain, Canine distemper, Marek’s disease vaccine, Foot and Mouth Disease, Gumboro, Mahepe/Mdondo/Kideri, Ndui, Pepopunda, Kimeta, Chambavu, Ugonjwa wa kutupa mimba kwa ng’ombe, Ugonjwa wa mapafu wa ng’ombe na mbuzi, Ugonjwa wa bonde la ufa, Ugonjwa wa ngozi (Lumpy skin, Streptothricosis, Warts, Mange) Ugonjwa wa miguu na midomo,

Maradhi yanayochanjwa na muda unaopendekezwa
  • Chanjo ya Gumboro kwa kuku wachanga mara moja katika uhai wake
  • Chanjo ya Mahepe/Mdondo/Kideri kwa kuku mara mbili katika uhai wake
  • Chanjo ya Ndui kwa kuku na ng’ombe mara moja;
  • Chanjo ya ugonjwa wa kutupa mimba kwa ng’ombe mara moja kwa mwaka
  • Chanjo ya ugonjwa wa Kimeta kwa ng’ombe kila mwaka;
  • Chanjo ya ugonjwa wa Chambavu kwa ng’ombe kila mwaka;
  • Chanjo ya ugonjwa wa pepopunda (Tetenasi ) kwa ng’ombe kila mwaka
  • Chanjo ya ugonjwa wa ngozi kwa ng’ombe, mbuzi na kondoo kila mwaka
  • Chanjo ya ugonjwa wa miguu na midomo kwa ng’ombe kila mwaka;
  • Chanjo ya ugonjwa wa homa ya mapafu kwa ng’ombe na mbuzi kila mwaka
  • Chanjo ya Kichaa cha mbwa kwa mbwa kila mwaka;
  • Chanjo ya ugonjwa wa matumbo hasa kwa mbwa wadogo pia unaweza kuchanja kwa wakubwa kila mwaka
  • Chanjo ya Ugonjwa wa sotoka kwa ng’ombe kila mwaka
  • Chanjo ya ugonjwa wa bonde la Ufa kwa ng’ombe;
  • Chanjo ya ugonjwa wa Farasi kwa farasi kila mwaka.
Wanyama wanaochanjwa
Wanyama hao ni pamoja na ng’ombe, mbuzi kondoo, nyati, ngamia, mbwa, paka, farasi na jamii ya ndege wakiwemo kuku wa aina zote wa mayai nyama na wa kienyeji.

Faida za Chanjo
  • Chanjo hudhibiti magonjwa yanayosababishwa na vimelea vya aina ya virusi, bektiria, rikesia na protozoa; 
  • Chanjo huongeza uwezo wa mnyama kujikinga na maradhi; 
  • Chanjo hulinda afya ya mifugo baada ya lishe bora na; 
  • Chanjo hudhibiti magonjwa yasiyoweza kutibika. 
Njia na sehemu za kuchanja
  • Kupitia mdomoni kwa magonjwa ya mahepe/mdondo/kideri, Gumboro kwa kuku; 
  • Kwenye bawa kwa ugonjwa wa ndui kwa kuku; 
  • Chini ya ngozi kwa magonjwa kama ya ngozi. 
Mambo ya kuzingatia katika uchanjaji
  1. Chanjo zihifadhiwe kwenye hali ya ubaridi na zisiwekwe kwenye joto au mwanga wa jua, wanyama wanaochanjwa ni lazima wawe na afya nzuri na hawajaambukizwa magonjwa yaliyokusudiwa kuchanjwa. Inashauriwa chanjo zifanywe na wataalamu wa mifugo au wafugaji waliopewa mafunzo ya kuchanja.
  2. Chanjo zinaweza kuleta madhara ikiwa zitatumiwa wakati muda wake wa matumizi umekwisha (expired).
  3. Aidha, chanjo zenye vijidudu vilivyohai zinaweza kuambukiza maradhi kwa wanyama waliochanjwa.

Comments

Popular posts from this blog

Utengenezaji wa Chakula cha Kuku wa Nyama (Bloilers)

Utangulizi Kuku wa nyama wana mahitaji yafuatayo ya viinilishe katika chakula ili wakue vizuri Viinilisha vya wanga 60-65%   Protini 30-35%   Madini 2-8% Chakula cha Vifaranga Chakula hiki hutengenezwa katika namna ya kumsaidia kifaranga aweze kumeza vizuri na hivyo hakitakiwi kuwa katika punje punje. Hata kama utanunua pumba, ni vema kuzipitisha kwenye mashine ili ziwe laini zaidi.  Mahitaji (kgs)  Unga wa dona wa nafaka kama mahindi au mtama 40  Pumba za mtama au mahindi au uwele 27  Mashudu ya alizeti au ufuta, au pamba au karanga n.k. 20  Unga wa mifupa au chokaa ya kuku (DCP) 2.25  Dagaa au mabaki ya samaki (sangara fish meal) 10  Chumvi ya jikoni 0.5  Virutubisho (Broiler premix) 0.25  Jumla utapata 100Kg. Chakula cha kukuzia – growers mash Mahitaji (Kg) Mahindi yaliyobarazwa au mtama au uwele 25   Pumba za mtama au mahindi au uwele 44   Mashudu ya alizeti au ufuta, au pamba au karanga n.k. 17   Unga wa mifupa au chokaa ya kuku (DCP) 3.25   Dagaa au mabaki ya samaki (fish meal) 1

Aina Za Miti ya Minazi

AINA ZA MINAZI Inafaa mkulima kufahamu kuna aina mbali mbali za minazi na ina mahitaji tofauti katika ukuaji. Ujuzi huu utamsaidia katika kuchagua aina ya minazi itakayofaa kwa eneo lake na kwa kiwango chake cha utunzaji. KUNA AINA TATU ZA MINAZI Minazi mirefu ya asili Minazi mifupi Minazi chotara MINAZI MIREFU YA ASILI (EAT) Minazi ya aina hii ndiyo inayojulikana na wakulima wengi kwa vile ni ya kiasili na imezoea mazingira yetu. Minazi hii huchukua miaka 6-8 tangu kupandikizwa hadi kuzaa. Minazi ya aina hii huvumilia ukame na inao uwezo wa kutoa wastani wa nazi 40 kwa mwaka. Nazi huwa kubwa na zenye nyama nene ambayo inafaa kwa kupikia na kukamua mafuta. Minazi hii huishi kad ya miaka 60 na kuendelea. Nchini Tanzania, minazi hii hustawi vyema ukanda wa pwani sehemu zisizo na mawe na ambazo hazituamishi maji. MINAZI MIFUPI (DWARF) Minazi ya aina hii huzaa mapema kuanzia miaka miwili. Huzaa nazi nyingi na ndogo. Nazi hizi huwa na nyama nyembamba hivyo hutumika kwa nnadafu. Minazi huhit

Kilimo cha Miti ya Mbao - Uwekezaji wa Muda wa Kati na Mrefu

Utangulizi Kilimo cha miti ni uwekezaji wa muda wa kati na mrefu (mid & long term investments). Ila kwa kawaida jamii nyingi hasa za kiafrika huwa hazivutiwi na uwekezaji wa muda mrefu. Hata hivyo kama una mpango wa kuwa imara kiuchumi inashauriwaau yakupasa kufikiria na kujifunza aina za uwekezaji wa muda mrefu. Miti hutumika kwa matumizi mengi mfano mbao, nguzo za umeme na kujengea, mapambo, kuni na mkaa, kuzalisha matunda, mitishamba na madawa,  utengenezeaji wa karatasi n.k.  Mchanganuo Ekari moja ya shamba unaweza kupanda miti mia sita (500) mpaka mia saba (700). Gharama za kununua mashamba au maeneo ya kupandia miti hutegemea na eneo. Kwa  sehemu nyingi za vijijini maeneo kwa ekari moja hayazidi laki 5.  Miche ya kununua mfano Mitiki huuzwa kuanzia elfu moja (1000) kwa mche mmoja Gharama ya kununua miche =  1000 * 600 = 600,000   Pia unaweza kuokoa gharama za kununua miche kwa kuioteshe mwenyewe ktk vitalu na kuiamishia shambani baada ya kustawi vizuri na kuwa imara.  Mf. Mbe