Skip to main content

Upandaji na Utunzaji wa Miti



a)      Kutayarisha shamba
Inapendekezwa kuwa pale inapowezekana shamba lilimwe kabisa kabla ya kupanda. Gharama ya kulima inaweza ikapunguzwa kwa kuchanganya miti na mazao ya kilimo, yaani kilimo mseto (Agroforestry) kama vile pamba, mahindi, mtama, tumbaku n.k  Utaratibu huu pia unapunguza gharama ya kupalilia. Miti mingine kama vile migriveria, mijohoro, miarobaini na mikenge inaweza kupandwa moja kwa moja katika mbuga mradi eneo kuzunguka shimo la kupandia mche limelimwa kabla ya kupanda.

b)     Majira ya kupanda
Kupanda miti kufanyike wakati wa mvua, yaani, wakati udongo una unyevuunyevu wa kutosha. Katika sehemu zenye mvua nyingi, ni rahisi kutekeleza jambo hili kwa sababu hali hiyo inaendelea kwa muda mrefu baada ya kuanza mvua za masika, wakati huo ni Machi na Aprili. Katika maeneo hayo inashauriwa kufuata majira yaleyale ya kupanda mazao ya chakula. Ni vizuri zaidi kupanda mara tu mvua za masika zinapoanza kunyesha.

Kutayarisha Mashimo ya Kupanda
Umbali kati  mti na mti hutegemea aina ya mti na madhumuni ya kuipanda. Iwapo madhumuni ni kuanzaisha shamba la miti (msitu) kwa kawaida umabli unaofaa ni mita 2.5 x 2.5 ambalo ni sawasawa na miti 1,600 kwa hekta 1. Kwa miti ambayo haikupandwa katika shamba la miti katika mtindo wa kilimo mseto, miti ipandwe kwa nafasi kufuatana na aina ya miti na matumizi, mfano: nguzo, malisho na uzio.  
Mashimo yenye upana wa Sm 30 (ft 1) na kina Sm 30 yachimbwe kwa mstari kwa kutumia kamba kisha miche isafirishwe kwa unagalifu kutoka katika bustani na kupandwa katika shimo mara moja, Kiriba lazima kiondolewe kabla ya kupanda. Wakati wa kupanda ni vyema kufukia mche kwa kutumia udongo kuzunguka mche ushindiliwe kwa uangalifu bila kukata mizizi ya mche.

Kutunza Shamba la Miti
a)      Kupalilia
Miti ya aina karibu zote haiwezi kuvumilia magugu. Isipopaliliwa mapema hudhoofika na hata kama baadaye ikipaliliwa itachukua muda mrefu kurudia hali yake ya awali. Miti mingine hufa kwa sababu ya magugu. Njia nzuri ya kuthibiti magugu ni kulima shamba vizuri kabla ya kupanda. Pale ambapo hakuna mazao ya kilimo, ni vyema kupalilia eneo lenye kipenyo cha m1 kuzunguka mti na pia kufyeka majani marefu kati ya miti.

b)     Kukatia matawi na kupunguza miti
Kwa baadhi ya miti ni vyema kukatia matawi ya chini katika kipindi cha miaka miwili ya mwanzo. Hii inasaidia wafanyakazi kupitia kwa urahisi katika shamba. Pia inazuia moto usisambae iwapo utatokea. Miti ya mbao kama vile msindano (Pine) na msanduku (Cypress) ina utaratibu maalumu uliowekwa (Pruning Schedule) wa kukatia matawi kulingana na umri na mahali ulipopandwa. Aina nyingi za miti hazina utaraibu maalumu wa kuipunguza, lakini kila mti uliokufa sharti uondolewe ili kutoa nafasi ya miti iliyo na afya. Pia miti ya msindano na msanduku ina utaratibu maalumu wa kupunguza miti (Thinning schedule). Zoezi hili hutegemeana na matumizi yaliyokusudiwa k.m kuni, mbao na karatasi n.k

Comments

Popular posts from this blog

How to Save Watermelon Seeds for Planting on Small Garden

Watermelon seeds from this year's garden can be planted next year. Seeds saved from the fruits of your garden's non-hybrid watermelon plants (Citrullus lanatus) can grow into new plants the following season. Different varieties of watermelons can cross-pollinate, which results in seedlings that aren't exactly like their parent plants. So grow only one watermelon variety in the garden if you want to save the seeds. The large seeds separate from the fruits easily, but they require some preparation to store well. Properly saved watermelon seeds can remain viable up to four years. Cut open a ripe watermelon. Scoop the seeds from the melon's flesh, and place them in a strainer. Rinse the seeds with warm tap water, removing most of the pulp. Add one drop of liquid dish soap, and wash the seeds gently to remove the remaining watermelon juice. Rinse the seeds thoroughly with only water. Spread the seeds on a sheet of wax paper. Dry the seeds for one week, turning them once each...

Kilimo Bora cha Alizeti - Uzalishaji, Uangalizi, Uvunaji na Uhifadhi

Utangulizi Alizeti hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Shinyanga, Singida, Dodoma, Iringa, Tabora, Morogoro, Ruvuma, Mbeya, Arusha, Manyara, na RukwaZao hili hulimwa kwa ajili ya chakula na biashara. Mambo muhimu ya kuzingatia wakati wa uzalishaji Kuchagua aina bora ya mbegu Chagua aina bora ya mbegu inayovumilia magonjwa, wadudu, inayotoa mazao mengi na kiwango kikubwa cha mafuta. Vilevile chagua aina ya mbegu ambayo hukomaa kwa wakati mmoja ili kurahisisha uvunaji. Kuweka mbolea Rutubisha udongo kwa kutumia mbolea za mboji na samadi ili kupata mazao mengi na bora. Kudhibiti wadudu na magonjwa Alizeti hushambuliwa na magonjwa ya majani, mizizi na masuke ambayo husababisha upungufu wa mavunoHivyo ni muhimu kuyadhibiti ili kupata mavuno mengi na boraPia ndege hupunguza mavuno kwa kiasi cha asilimia 50 au zaidiNjia ya kudhibiti ndege ni kwa kuwafukuza na kupanda mbegu zinazokomaa mapema. Maandalizi kabla ya kuvuna;  Ukaguzi  Kagua shamba kuona kama alizeti imekomaaAlizeti hukomaa ...

Agriculture in Tanzania

Introduction Agriculture is main part of Tanzania's economy. As of 2016 Tanzania has over 44 million hectares of arable land with only 33% of this amount being cultivated. More than 80% of the poor population live in rural areas and almost all of them are involved in the farming sector Land is a vital asset in ensuring food security and among the main food crops in Tanzania are maize, sorghum, millet, rice, wheat, beans, cassava, potatoes and bananas. Agricultural products also contributes largely to the country's foreign exchange earnings and over 1 billion dollars is earning from cash crop exports. Cash crops include Coffee, Sisal, Cashew nut, Tea, Cotton and Tobacco. At one point in history Tanzania was the largest producer of sisal in the world. The agriculture sector faces various challenges and has been the governments top priority to develop to reduce poverty.Farming efficiently has been a challenge of many farmers and lack of finances and lack of farming education has l...