Skip to main content

Upandaji na Utunzaji wa Miti



a)      Kutayarisha shamba
Inapendekezwa kuwa pale inapowezekana shamba lilimwe kabisa kabla ya kupanda. Gharama ya kulima inaweza ikapunguzwa kwa kuchanganya miti na mazao ya kilimo, yaani kilimo mseto (Agroforestry) kama vile pamba, mahindi, mtama, tumbaku n.k  Utaratibu huu pia unapunguza gharama ya kupalilia. Miti mingine kama vile migriveria, mijohoro, miarobaini na mikenge inaweza kupandwa moja kwa moja katika mbuga mradi eneo kuzunguka shimo la kupandia mche limelimwa kabla ya kupanda.

b)     Majira ya kupanda
Kupanda miti kufanyike wakati wa mvua, yaani, wakati udongo una unyevuunyevu wa kutosha. Katika sehemu zenye mvua nyingi, ni rahisi kutekeleza jambo hili kwa sababu hali hiyo inaendelea kwa muda mrefu baada ya kuanza mvua za masika, wakati huo ni Machi na Aprili. Katika maeneo hayo inashauriwa kufuata majira yaleyale ya kupanda mazao ya chakula. Ni vizuri zaidi kupanda mara tu mvua za masika zinapoanza kunyesha.

Kutayarisha Mashimo ya Kupanda
Umbali kati  mti na mti hutegemea aina ya mti na madhumuni ya kuipanda. Iwapo madhumuni ni kuanzaisha shamba la miti (msitu) kwa kawaida umabli unaofaa ni mita 2.5 x 2.5 ambalo ni sawasawa na miti 1,600 kwa hekta 1. Kwa miti ambayo haikupandwa katika shamba la miti katika mtindo wa kilimo mseto, miti ipandwe kwa nafasi kufuatana na aina ya miti na matumizi, mfano: nguzo, malisho na uzio.  
Mashimo yenye upana wa Sm 30 (ft 1) na kina Sm 30 yachimbwe kwa mstari kwa kutumia kamba kisha miche isafirishwe kwa unagalifu kutoka katika bustani na kupandwa katika shimo mara moja, Kiriba lazima kiondolewe kabla ya kupanda. Wakati wa kupanda ni vyema kufukia mche kwa kutumia udongo kuzunguka mche ushindiliwe kwa uangalifu bila kukata mizizi ya mche.

Kutunza Shamba la Miti
a)      Kupalilia
Miti ya aina karibu zote haiwezi kuvumilia magugu. Isipopaliliwa mapema hudhoofika na hata kama baadaye ikipaliliwa itachukua muda mrefu kurudia hali yake ya awali. Miti mingine hufa kwa sababu ya magugu. Njia nzuri ya kuthibiti magugu ni kulima shamba vizuri kabla ya kupanda. Pale ambapo hakuna mazao ya kilimo, ni vyema kupalilia eneo lenye kipenyo cha m1 kuzunguka mti na pia kufyeka majani marefu kati ya miti.

b)     Kukatia matawi na kupunguza miti
Kwa baadhi ya miti ni vyema kukatia matawi ya chini katika kipindi cha miaka miwili ya mwanzo. Hii inasaidia wafanyakazi kupitia kwa urahisi katika shamba. Pia inazuia moto usisambae iwapo utatokea. Miti ya mbao kama vile msindano (Pine) na msanduku (Cypress) ina utaratibu maalumu uliowekwa (Pruning Schedule) wa kukatia matawi kulingana na umri na mahali ulipopandwa. Aina nyingi za miti hazina utaraibu maalumu wa kuipunguza, lakini kila mti uliokufa sharti uondolewe ili kutoa nafasi ya miti iliyo na afya. Pia miti ya msindano na msanduku ina utaratibu maalumu wa kupunguza miti (Thinning schedule). Zoezi hili hutegemeana na matumizi yaliyokusudiwa k.m kuni, mbao na karatasi n.k

Comments

Popular posts from this blog

Utengenezaji wa Chakula cha Kuku wa Nyama (Bloilers)

Utangulizi Kuku wa nyama wana mahitaji yafuatayo ya viinilishe katika chakula ili wakue vizuri Viinilisha vya wanga 60-65%   Protini 30-35%   Madini 2-8% Chakula cha Vifaranga Chakula hiki hutengenezwa katika namna ya kumsaidia kifaranga aweze kumeza vizuri na hivyo hakitakiwi kuwa katika punje punje. Hata kama utanunua pumba, ni vema kuzipitisha kwenye mashine ili ziwe laini zaidi.  Mahitaji (kgs)  Unga wa dona wa nafaka kama mahindi au mtama 40  Pumba za mtama au mahindi au uwele 27  Mashudu ya alizeti au ufuta, au pamba au karanga n.k. 20  Unga wa mifupa au chokaa ya kuku (DCP) 2.25  Dagaa au mabaki ya samaki (sangara fish meal) 10  Chumvi ya jikoni 0.5  Virutubisho (Broiler premix) 0.25  Jumla utapata 100Kg. Chakula cha kukuzia – growers mash Mahitaji (Kg) Mahindi yaliyobarazwa au mtama au uwele 25   Pumba za mtama au mahindi au uwele 44   Mashudu ya alizeti au ufuta, au pamba au karanga n.k. 17   Unga wa mifupa a...

Kilimo cha Miti ya Mbao - Uwekezaji wa Muda wa Kati na Mrefu

Utangulizi Kilimo cha miti ni uwekezaji wa muda wa kati na mrefu (mid & long term investments). Ila kwa kawaida jamii nyingi hasa za kiafrika huwa hazivutiwi na uwekezaji wa muda mrefu. Hata hivyo kama una mpango wa kuwa imara kiuchumi inashauriwaau yakupasa kufikiria na kujifunza aina za uwekezaji wa muda mrefu. Miti hutumika kwa matumizi mengi mfano mbao, nguzo za umeme na kujengea, mapambo, kuni na mkaa, kuzalisha matunda, mitishamba na madawa,  utengenezeaji wa karatasi n.k.  Mchanganuo Ekari moja ya shamba unaweza kupanda miti mia sita (500) mpaka mia saba (700). Gharama za kununua mashamba au maeneo ya kupandia miti hutegemea na eneo. Kwa  sehemu nyingi za vijijini maeneo kwa ekari moja hayazidi laki 5.  Miche ya kununua mfano Mitiki huuzwa kuanzia elfu moja (1000) kwa mche mmoja Gharama ya kununua miche =  1000 * 600 = 600,000   Pia unaweza kuokoa gharama za kununua miche kwa kuioteshe mwenyewe ktk vitalu na kuiamishia shambani baada ya kustawi v...

Uandaaji na Uoteshaji wa Mbegu za Mitiki

Utangulizi Mbegu za mitiki zinapatikana Tanzania Tree Seed Agency wako Msamvu Morogoro.Kilo moja ya mbegu za mitiki inatosha kuotesha kwenye shamba la hekta moja, ambayo ni wastani wa miti 1500 Matayarisho: Ganda la nje la mbengu ya mtiki ni gumu sana na lina sumu mbaya.Unatakiwa uloweke mbegu ya mitiki kwa masaa 72, na kila baada ya masaa 12 unatakiwa ubadilishe maji kwa kumwaga maji ya zamani na kuweka maji mapya. Baada ya masaa 72 anika mbegu zako juani kwa masaa 12 (zianikike ktk bati). Tengeneza kitalu, weka mbolea ya wanyama au mboji, kisha panda mbegu zako kwenye kitalu. Mwangilia maji kila siku asubuhi na jioni, mbegu zitaanza kuota baada ya siku 10 hadi 20. Miche ikifikia urefu wa futi moja, unaweza sasa kuiotesha kwenye shamba lako ulilotayarisha kwa ajili ya kuotesha miti. Kabla ya kung’'oa miche hakikisha unamwaga maji mengi, ili mizizi isikatike sana, kisha chukua kisu chenye makali ya kutosha na kata ncha ya juu ya mti na ondoa majani, hii inasaidia mti kuchipuka upya...