Skip to main content

Kutunza Bustani Kwaweza Kukunufaisha

JE, WEWE hufurahia kutunza bustani? Huenda unanufaika hata zaidi kutokana na utendaji huo. Kulingana na gazeti moja la London (Independent), watafiti wamegundua kwamba “kutunza bustani hukusaidia kuwa na afya nzuri zaidi, hupunguza mifadhaiko, hushusha shinikizo la damu na hata kukusaidia kuishi kwa muda mrefu zaidi.”
Mhariri G. Search anasema: “Baada ya siku yenye shughuli nyingi na mambo mengi yenye kufadhaisha, kurudi nyumbani na kutunza bustani yako huburudisha sana.” Mbali na kuwa jambo lenye kuthawabisha na kupendeza, kutunza bustani kunakuwezesha kupata mazoezi mazuri zaidi ya mwili kuliko kwenda katika chumba cha mazoezi. Jinsi gani? Kulingana na Search, “utendaji kama vile kulima na kukusanya majani ni mazoezi mazuri yanayotumia kalori nyingi zaidi kuliko kuendesha baiskeli.”
Kutunza bustani huwanufaisha hasa wazee. Kusubiri chipukizi au mche mpya uibuke huwasaidia kutazamia wakati ujao wakiwa na uhakika. Pia, “bustani hutuliza maumivu na mfadhaiko” unaosababishwa na uzee, asema Dakt. Brigid Boardman wa Royal Horticultural Society. Mara nyingi wazee huvunjika moyo kwa sababu ya kuwategemea sana wengine. Hata hivyo, kama Dakt. Boardman anavyosema, “ile hisia ya kutaka kujitegemea inatoshelezwa kwa kuamua kitakachopandwa, mahali kitakapopandwa, na jinsi ya kuitunza bustani. Na ule uhitaji wa kutunza unatoshelezwa pia.”
Wale walio na matatizo ya akili mara nyingi hutulia wanapofanya kazi katika mazingira mazuri, matulivu. Isitoshe, kupanda maua au chakula kwa ajili ya wengine kwaweza kuwasaidia watu hao wajiamini tena na kujiheshimu.
Hata hivyo, wanaofaidika na bustani hizo si wale wanaozitunza tu. Profesa Roger Ulrich wa Chuo Kikuu cha Texas alifanya majaribio kwa kutumia kikundi cha watu waliokuwa wametiwa chini ya mkazo. Aligundua kwamba wale waliopelekwa mahali penye miti na majani mengi walipata nafuu haraka—kulingana na mpigo wa moyo na shinikizo la damu—kuliko wale ambao hawakuwekwa katika mazingira hayo ya asili. Jaribio kama hilo lilionyesha kwamba wagonjwa wanaoendelea kupata nafuu katika hospitali baada ya kufanyiwa upasuaji walinufaika kwa kukaa katika vyumba ambamo wangeweza kuona miti. Tofauti na wagonjwa wengine, “walipata nafuu haraka, wakarudi nyumbani mapema, hawakuhitaji dawa nyingi za kutuliza maumivu, na walikuwa na malalamiko machache zaidi.”

Comments

Popular posts from this blog

Utengenezaji wa Chakula cha Kuku wa Nyama (Bloilers)

Utangulizi Kuku wa nyama wana mahitaji yafuatayo ya viinilishe katika chakula ili wakue vizuri Viinilisha vya wanga 60-65%   Protini 30-35%   Madini 2-8% Chakula cha Vifaranga Chakula hiki hutengenezwa katika namna ya kumsaidia kifaranga aweze kumeza vizuri na hivyo hakitakiwi kuwa katika punje punje. Hata kama utanunua pumba, ni vema kuzipitisha kwenye mashine ili ziwe laini zaidi.  Mahitaji (kgs)  Unga wa dona wa nafaka kama mahindi au mtama 40  Pumba za mtama au mahindi au uwele 27  Mashudu ya alizeti au ufuta, au pamba au karanga n.k. 20  Unga wa mifupa au chokaa ya kuku (DCP) 2.25  Dagaa au mabaki ya samaki (sangara fish meal) 10  Chumvi ya jikoni 0.5  Virutubisho (Broiler premix) 0.25  Jumla utapata 100Kg. Chakula cha kukuzia – growers mash Mahitaji (Kg) Mahindi yaliyobarazwa au mtama au uwele 25   Pumba za mtama au mahindi au uwele 44   Mashudu ya alizeti au ufuta, au pamba au karanga n.k. 17   Unga wa mifupa a...

Uandaaji na Uoteshaji wa Mbegu za Mitiki

Utangulizi Mbegu za mitiki zinapatikana Tanzania Tree Seed Agency wako Msamvu Morogoro.Kilo moja ya mbegu za mitiki inatosha kuotesha kwenye shamba la hekta moja, ambayo ni wastani wa miti 1500 Matayarisho: Ganda la nje la mbengu ya mtiki ni gumu sana na lina sumu mbaya.Unatakiwa uloweke mbegu ya mitiki kwa masaa 72, na kila baada ya masaa 12 unatakiwa ubadilishe maji kwa kumwaga maji ya zamani na kuweka maji mapya. Baada ya masaa 72 anika mbegu zako juani kwa masaa 12 (zianikike ktk bati). Tengeneza kitalu, weka mbolea ya wanyama au mboji, kisha panda mbegu zako kwenye kitalu. Mwangilia maji kila siku asubuhi na jioni, mbegu zitaanza kuota baada ya siku 10 hadi 20. Miche ikifikia urefu wa futi moja, unaweza sasa kuiotesha kwenye shamba lako ulilotayarisha kwa ajili ya kuotesha miti. Kabla ya kung’'oa miche hakikisha unamwaga maji mengi, ili mizizi isikatike sana, kisha chukua kisu chenye makali ya kutosha na kata ncha ya juu ya mti na ondoa majani, hii inasaidia mti kuchipuka upya...

Kilimo cha Miti ya Mbao - Uwekezaji wa Muda wa Kati na Mrefu

Utangulizi Kilimo cha miti ni uwekezaji wa muda wa kati na mrefu (mid & long term investments). Ila kwa kawaida jamii nyingi hasa za kiafrika huwa hazivutiwi na uwekezaji wa muda mrefu. Hata hivyo kama una mpango wa kuwa imara kiuchumi inashauriwaau yakupasa kufikiria na kujifunza aina za uwekezaji wa muda mrefu. Miti hutumika kwa matumizi mengi mfano mbao, nguzo za umeme na kujengea, mapambo, kuni na mkaa, kuzalisha matunda, mitishamba na madawa,  utengenezeaji wa karatasi n.k.  Mchanganuo Ekari moja ya shamba unaweza kupanda miti mia sita (500) mpaka mia saba (700). Gharama za kununua mashamba au maeneo ya kupandia miti hutegemea na eneo. Kwa  sehemu nyingi za vijijini maeneo kwa ekari moja hayazidi laki 5.  Miche ya kununua mfano Mitiki huuzwa kuanzia elfu moja (1000) kwa mche mmoja Gharama ya kununua miche =  1000 * 600 = 600,000   Pia unaweza kuokoa gharama za kununua miche kwa kuioteshe mwenyewe ktk vitalu na kuiamishia shambani baada ya kustawi v...