Skip to main content

Dawa za Asili za Mimea (Kuzia Wadudu Waharibifu wa Mazao)

Unaweza kutumia mimea fulani kupunguza idadi ya wadudu waharibifu shambani mwako. Panda mimea ambayo huepukwa na wadudu waharibifu karibu na mimea inayohitaji kulindwa. Kwa mfano, minyoo fulani ambayo hula na kudhoofisha mizizi ya mimea mingi haiwezi kukaribia mimea ya matageta. Na vipepeo fulani ambao huharibu kabichi hawakaribii kabichi zilizopandwa karibu na mimea ya rosemary, sage, au thyme.Hata hivyo, tahadhari hii yafaa: Mimea fulani huwavutia wadudu waharibifu.
JINATIBA UTUMIAJI
MnyaaKuua MchwaMatone 10 ya mnyaa + maji lita moja. Koroga. Nyunyuzia/ Pulizia kwenye mchwa
UtupaWadudu wanaoshambulia mboga Twanga kiganja kimoja cha majani. Loweka kwenye lita 1 ya maji kwa masaa 24. Chuja. Ongeza 1/8 ya kipande cha mche wa sabuni. Pulizia kwenye mboga
Muarobaini – MajaniWadudu wa mboga Ponda ganja mkona 1 wa majani. Changanya kwenye lita 1 ya maji. Loweka kwa siku mbili , halafu ongeza sabuni 1/8 ya kipande mche. Nyunyuzia kwenye mboga.
Muarobaini - Mbegu Wadudu wanaoshambulia mboga Twanga mbegu kilo 5 (kisado kimajo). Loweka kwenye maji lita 15 kwa masaa 24. Chuja na pulizia/ nyunyuzia kwenye mboga
PapaiKuua mchwa Ponda majani laini ya mpapai. Ongeza lita 1 ya maji. Chuja na pulizia/ nyunyuzia kwenye mchwa
Bangi Mwitu Kuhifadhi vyakula vya nafaka (food grains)Sambaza halafu weka gunia juu yake. Endelea hivyo hivyo.
Mkojo wa n’gombe Kuua mchwa/ wadudu wa mboga Uache mkojo kwa siku 10 –14. Kwa kila lita 1 ya mkojo ongeza lita 2 za maji na 1/8 sabuni ya mche. Nyunyuzia kwenye mchwa au mboga
Mnanaa (mbarika mwitu) Kuua wadudu wanaoshambulia mboga Gram 100 mbegu + lita 1 maji + 1/8 sabuni mche. Pulizia/ nyunyizia kwenye mboga
Kitunguu saumuKuua wadudu wanaoshambulia mbogaGram 100 (3-4) twanga. Ongezea lita 1 ya maji. Acha kwa saa 24. Chuja na ongeza 1/8 ya kipande cha mche wa sabuni. Pulizia/ Nyunyuzia kwenye wadudu
Pilipili KaliKuua wadudu kwenye mboga Changanya vijiko 3 vya chakula na lita 1 ya maji. Acha kwa saa 12. Ongezea 1/8 ya kipande cha sabuni mche. Nyunyizia kwenye mimea
Mashona nguo Kuua waduduChemsha mbegu kikombe 1 na lita 1 ya maji kwa dakika 10 au loweka siku moja na ongezea 1/8 ya kipande cha sabuni mche. Nyunyuzia kwenye mboga
Muarobaini Kideri (New Castle disease) Twanga majani 1kg, ongeza maji lita 1. Wanyweshe kuku asubui. Fanya hivi kila mwezi
Majivu Kuua wadudu mafuta (aphids) Nyunyizia majivu kwenye wadudu wanaoshambulia mboga
Majivu Kuhifadhi mazao Changanya majivu + pilipili kichaa + Cyprus. Sambaza kwenye gunia halafu weka gunia juu yake. Endelea hivyo hivyo.
Marejea Mbolea Panda shambani na baadaye limia chini ardhini

Comments

  1. naomba kuuliza mbolea ya kuku inakaa baada ya muda gani kabla ya kupanda mchicha? maana niliweka mbolea saatano nililushia mbegu saa kumi na moja zikaungua naomba Elimu

    ReplyDelete
    Replies
    1. Mbolea ya kuku inatakiwa kuwekwa shambani endapo itakuwa full decomposed (imeiva vizuri).Na inatakiwa ikae angalau wiki moja shambani kabla ya kusia au kupanda mazao

      Delete
  2. Dawa gani za asili za kuua wadudu pilipili kichaa zangu zina waiki mbili sasa

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

Kanuni za Ufugaji Bora wa Mbuzi na Kondoo

Utangulizi Mbuzi na kondoo wanaweza kufugwa kwa gharama nafuu na kuishi katika mazingira magumu kama ya maradhi na ukame ikilinganishwa na ng’ombe. Kutokana na umbile lao dogo wanaweza kufugwa katika eneo dogo na pia wanaweza kuhudumiwa na familia yenye nguvukazi na kipato kidogo. Uzao wa muda mfupi unamwezesha mfugaji kupata mbuzi/kondoo wengi kwa kipindi kifupi. Wanyama hao hufugwa kwa ajili ya nyama, maziwa, ngozi, sufu na mazao mengine kwa matumizi ya familia na kuongeza kipato.  Kanuni za kuzingatia Ufugaji bora wa mbuzi na kondoo uzingatie kanuni zifuatazo:- Wafugwe kwenye banda au zizi bora, Wachaguliwe kutokana na sifa za koo/aina na lengo la uzalishaji (nyama, maziwa au sufu), Wapatiwe lishe sahihi kulingana na umri na mahitaji ya mwili, Kuzingatia mbinu za kudhibiti magonjwa kama inavyoshauriwa na mtaalam wa mifugo, Kuweka na kutunza kumbukumbu sahihi za uzalishaji; na  Kuzalisha nyama, maziwa au sufu yenye ubora unaokidhi mahitaji ya soko Zizi au Banda la Mbuzi/Kond...

Kilimo Bora cha Alizeti - Uzalishaji, Uangalizi, Uvunaji na Uhifadhi

Utangulizi Alizeti hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Shinyanga, Singida, Dodoma, Iringa, Tabora, Morogoro, Ruvuma, Mbeya, Arusha, Manyara, na RukwaZao hili hulimwa kwa ajili ya chakula na biashara. Mambo muhimu ya kuzingatia wakati wa uzalishaji Kuchagua aina bora ya mbegu Chagua aina bora ya mbegu inayovumilia magonjwa, wadudu, inayotoa mazao mengi na kiwango kikubwa cha mafuta. Vilevile chagua aina ya mbegu ambayo hukomaa kwa wakati mmoja ili kurahisisha uvunaji. Kuweka mbolea Rutubisha udongo kwa kutumia mbolea za mboji na samadi ili kupata mazao mengi na bora. Kudhibiti wadudu na magonjwa Alizeti hushambuliwa na magonjwa ya majani, mizizi na masuke ambayo husababisha upungufu wa mavunoHivyo ni muhimu kuyadhibiti ili kupata mavuno mengi na boraPia ndege hupunguza mavuno kwa kiasi cha asilimia 50 au zaidiNjia ya kudhibiti ndege ni kwa kuwafukuza na kupanda mbegu zinazokomaa mapema. Maandalizi kabla ya kuvuna;  Ukaguzi  Kagua shamba kuona kama alizeti imekomaaAlizeti hukomaa ...

Utengenezaji wa Chakula cha Kuku wa Nyama (Bloilers)

Utangulizi Kuku wa nyama wana mahitaji yafuatayo ya viinilishe katika chakula ili wakue vizuri Viinilisha vya wanga 60-65%   Protini 30-35%   Madini 2-8% Chakula cha Vifaranga Chakula hiki hutengenezwa katika namna ya kumsaidia kifaranga aweze kumeza vizuri na hivyo hakitakiwi kuwa katika punje punje. Hata kama utanunua pumba, ni vema kuzipitisha kwenye mashine ili ziwe laini zaidi.  Mahitaji (kgs)  Unga wa dona wa nafaka kama mahindi au mtama 40  Pumba za mtama au mahindi au uwele 27  Mashudu ya alizeti au ufuta, au pamba au karanga n.k. 20  Unga wa mifupa au chokaa ya kuku (DCP) 2.25  Dagaa au mabaki ya samaki (sangara fish meal) 10  Chumvi ya jikoni 0.5  Virutubisho (Broiler premix) 0.25  Jumla utapata 100Kg. Chakula cha kukuzia – growers mash Mahitaji (Kg) Mahindi yaliyobarazwa au mtama au uwele 25   Pumba za mtama au mahindi au uwele 44   Mashudu ya alizeti au ufuta, au pamba au karanga n.k. 17   Unga wa mifupa a...