Skip to main content

Kilimo cha Mboga, Matunda Kinavyoweza Kukuza Uchumi


KILIMO ni kilimo tu iwe mjini au vijijini ilimradi kimnufaishe mkulima na kupata faida kwa kile alichoamua kuzalisha.

Makala haya yanajikita kwenye kilimo ambacho wengi wanaweza kushangaa kwa sababu ya asili ya kilimo chenyewe. Ukitaja neno kilimo wengi hukifikiria kilimo cha mashambani hasa vijijini. Kilimo ninachokizungumzia ni cha mboga zikiwemo hoho, nyanya, biringanya, vitunguu, kabeji, matembele na mchicha. Kilimo hiki kinaweza kufanyika katika njia kuu mbili: kwanza ni kwa kutumia njia ijulikanayo kama ‘green house’ na kilimo cha wazi ambacho hufanyika katika maeneo maalumu ya wazi ambayo serikali inatakiwa iyaweke inapopanga mipangilio ya miji.

Katika kufahamu undani wa kilimo hiki, mwandishi wa makala haya amefanya mahojiano na Mtaalamu wa Mipango Miji na Mhadhiri Msaidizi kutoka Chuo Kikuu cha Ardhi, Hussein Kayera. Kwanza anaeleza historia ya kilimo hiki cha mboga mijini Tanzania na namna wananchi wanavyoweza kunufaika na shughuli hizo. Kayera anasema, kilimo cha mboga mijini kipo kwa mujibu wa sheria lakini hakuna maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya shughuli hizo.

Kwa mujibu wa Kayera, kilimo cha mboga mijini kiliruhusiwa rasmi na serikali mwaka 1970 na kuzuiliwa mwaka 1980 kabla ya kurejeshwa tena rasmi mwaka 2000. Anasema, kilimo hicho kinaweza kuzalisha mboga kama vile nyanya, biringanya, hoho, mchicha, matembele na nyanya chungu.

“Kilimo cha mboga mijini ni kizuri sana na pia kipo kwa mujibu wa sheria lakini serikali ndiyo imeshindwa kutenga maeneo maalumu kwa ajili ya shughuli hizo za kilimo” “Serikali ilitakiwa itenge maeneo tangu mwaka 2000 ilipopitisha sheria ya kutambua kilimo cha mijini, lakini hakuna juhudi zozote zilizofanyika na badala yake wananchi wanajilimia kando kando ya mito na mifereji ya maji machafu yanayotoka viwandani ambayo huhatarisha afya,” anasema Kayera.

Kayera anasema, kilimo hicho kinakabiliwa na changamoto kadhaa ukiwemo ukosefu wa maeneo maalumu yaliyotengwa na serikali kwa ajili ya kufanyia shughuli hizo za uzalishaji wa mboga. Anataja changamoto nyingine kuwa ni kutokuwa na uhakika wa kumiliki eneo mijini kwa ajili ya kilimo na pia wakulima wanatumia maji machafu ambayo ni hatari kiafya. Anasema, baadhi ya wakulima wa kilimo hicho mijini hutumia viuatilifu bila ya kufuata taratibu, kitu ambacho husababisha madhara makubwa kiafya.

Kayera anasema, utumiaji wa ardhi na maji yasiyokuwa salama unaweza kusababisha uzalishaji wa mazao yasiyokuwa salama na hivyo huhatarisha afya za walaji. Changamoto nyingine inayotajwa kuwakabili wakulima wa mboga mijini ni ukosefu wa soko la kimataifa na ugumu wa hifadhi za mboga ili zikae muda mrefu bila kuharibika. Kayera anasema, kilimo hicho kikipewa kipaumbele kitasaidia kupunguza tatizo la ajira, kitaongeza uzalishaji wa mboga bora ambazo hazina kemikali ukilinganisha na zile zinazozalishwa kwenye mifereji ya maji machafu yatokayo viwandani.

Mkulima wa mboga katika eneo la Msimbazi jijini Dar es Salaam, Janeth Mlinga, anasema kilimo hicho ndicho kinachoendesha maisha yake. Kwa muda mrefu, kumekuwa na tuhuma kwamba, mboga zinazozalishwa katika bonde la mto Msimbazi ni hatari kwa afya kwa muwa wakulima wanatumia maji yenye kemikali yanayotoka viwandani.

“Kilimo hiki ni kizuri sana kwani ndio msingi wa maisha ya familia yangu, napata hapa chakula na mahitaji ya kila siku ya familia yangu japokuwa wengi yanasema kuwa mboga zinazozalishwa hapa ni mbaya na zina madhara kwa afya, hii sio kweli kwani sijasikia mtu aliyekufa kwa kula mboga zilizozalishwa katika bonde hili,” anasema Mlinga. Inadaiwa kuwa, kama wananchi wengi wa mkoa wa Dar es Salaam wangekuwa wanatembelea maeneo zinapozalishwa mbogamboga wanazokula wangeendelea kuzila kwa sababu zinalimwa kwenye mazingira machafu, na maji yanayotumika kumwagilia pia yanakatisha tamaa.

Mlinga anasema, yeye ameanza kulima mchicha, matembele na bamia katika bonde hilo kwa miaka zaidi ya 10 sasa na hajawahi kupata kesi wala kusikia kutoka hospitalini kuwa kuna mtu amefariki dunia kutokana na kutumia mboga zilizotoka bonde la Msimbazi. “Mboga tunazozalisha sisi hapa ni nzuri kiafya na pia hata wenyewe tunakula, hivyo kama tunazalisha chakula ambacho hata sisi wenyewe tunatumia, ujue tunazailisha kitu chenye ubora,” anasema Mlinga.

Utafiti uliofanywa na Chuo Kikuu cha Ardhi katika bonde la mto Msimbazi ukijumuisha udongo na maji katika bonde hilo kwa kuzingatia vigezo vya Shirika la Afya dunia WHO na Shirika la viwango nchini TBS, umebaini uwepo wa kemikali na sumu. Utafiti huo uligundua kuwa maeneo mengine yanayotumika kwa ajili ya kilimo cha mbogamboga hutumika kwa kutupia takataka zikiwemo betri zilizoisha muda wa matumizi, masalia ya simu za mkononi, vipuri vya magari na majokofu mabovu.

Taka hizo zenye sumu hutupwa kwenye mifereji ya maji yanayotumika kwa umwagiliaji wa mboga na hivyo kuhatarisha afya za walaji. Katika utafiti huo, imebainika kuwa mboga zinazomwagiliwa na maji yenye sumu pamoja na kemikali yakiwemo madini ya risasi, shaba na kromiamu ni hatari kwa afya ya binadamu.

Utafiti huo unaonesha kuwa mboga zinazozalishwa katika bonde la Msimbazi huuzwa katika masoko ya Ilala, Kariakoo, Buguruni, Veterani, Tazara, Mwananyamala, Mnyamani, Kigogo, Kisutu, Vingunguti, Tabata, Mikoroshini na maeneo ya jirani na wakulima hao mkoani Dar es Salaam.

IMEANDIKWA NA EMMANUEL GHULA - HABARILEO

Comments

Popular posts from this blog

How to Save Watermelon Seeds for Planting on Small Garden

Watermelon seeds from this year's garden can be planted next year. Seeds saved from the fruits of your garden's non-hybrid watermelon plants (Citrullus lanatus) can grow into new plants the following season. Different varieties of watermelons can cross-pollinate, which results in seedlings that aren't exactly like their parent plants. So grow only one watermelon variety in the garden if you want to save the seeds. The large seeds separate from the fruits easily, but they require some preparation to store well. Properly saved watermelon seeds can remain viable up to four years. Cut open a ripe watermelon. Scoop the seeds from the melon's flesh, and place them in a strainer. Rinse the seeds with warm tap water, removing most of the pulp. Add one drop of liquid dish soap, and wash the seeds gently to remove the remaining watermelon juice. Rinse the seeds thoroughly with only water. Spread the seeds on a sheet of wax paper. Dry the seeds for one week, turning them once each...

Kilimo Bora cha Alizeti - Uzalishaji, Uangalizi, Uvunaji na Uhifadhi

Utangulizi Alizeti hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Shinyanga, Singida, Dodoma, Iringa, Tabora, Morogoro, Ruvuma, Mbeya, Arusha, Manyara, na RukwaZao hili hulimwa kwa ajili ya chakula na biashara. Mambo muhimu ya kuzingatia wakati wa uzalishaji Kuchagua aina bora ya mbegu Chagua aina bora ya mbegu inayovumilia magonjwa, wadudu, inayotoa mazao mengi na kiwango kikubwa cha mafuta. Vilevile chagua aina ya mbegu ambayo hukomaa kwa wakati mmoja ili kurahisisha uvunaji. Kuweka mbolea Rutubisha udongo kwa kutumia mbolea za mboji na samadi ili kupata mazao mengi na bora. Kudhibiti wadudu na magonjwa Alizeti hushambuliwa na magonjwa ya majani, mizizi na masuke ambayo husababisha upungufu wa mavunoHivyo ni muhimu kuyadhibiti ili kupata mavuno mengi na boraPia ndege hupunguza mavuno kwa kiasi cha asilimia 50 au zaidiNjia ya kudhibiti ndege ni kwa kuwafukuza na kupanda mbegu zinazokomaa mapema. Maandalizi kabla ya kuvuna;  Ukaguzi  Kagua shamba kuona kama alizeti imekomaaAlizeti hukomaa ...

Agriculture in Tanzania

Introduction Agriculture is main part of Tanzania's economy. As of 2016 Tanzania has over 44 million hectares of arable land with only 33% of this amount being cultivated. More than 80% of the poor population live in rural areas and almost all of them are involved in the farming sector Land is a vital asset in ensuring food security and among the main food crops in Tanzania are maize, sorghum, millet, rice, wheat, beans, cassava, potatoes and bananas. Agricultural products also contributes largely to the country's foreign exchange earnings and over 1 billion dollars is earning from cash crop exports. Cash crops include Coffee, Sisal, Cashew nut, Tea, Cotton and Tobacco. At one point in history Tanzania was the largest producer of sisal in the world. The agriculture sector faces various challenges and has been the governments top priority to develop to reduce poverty.Farming efficiently has been a challenge of many farmers and lack of finances and lack of farming education has l...