Skip to main content

Kilimo cha Pilipili Hoho na Manga



Utangulizi
Pilipili ni kiungo kikali, hutumiwa kwa kukoleza mchuzi na vyakula mbali mbali. Pilipili zinaweza kupikwa zikiwa nzima au kukatwakatwa na kutumiwa katika kachumbari; au kuwekwa kwenye siki na achali, au kusagwa na kutumia unga wake.
Hili ni zao la nchi za kitropiki, na hutumiwa sana na wakazi wa Bara Hindi, Mashariki ya Mbali. Amerika ya Kusini na Afrika ya Tropiki. Pilipili huwekwa katika makundi makubwa mawili, yaani:
  1.  Pilipili Hoho (Hot Pepper)- Hizi ni ndogo ndogo, ndefu, nyembamba, na kali sana. Aina zinazojulikana zaidi ni Green Chilli, Cherry Pepper, Long Cayenne na Tabasco.
  2. Pilipili Manga (Sweet Pepper)- Hizi zina umbo kubwa, nyama nying, mviringo na ndefu kidogo, siyo kali. Aina zinazojulikana zaidi ni Sweet, Neapolitan, Keystone, Giant, Ynlo Wonder na california wonder.
Kupanda
Mbegu hupandwa kwenye kitalu ambamo hukaa kwa muda wa majuma manane hadi kumi. Kisha miche hupandikizwa bustani kwa umbali wa sentimeta 45 kwa 90.

Kuvuna
Umri wa kuvuna zao hili hutegemea aina ya pilipili na matumizi yake. Aina ambayo ni kubwa na tamu kwa kawaida huvunwa kabla haijapevuka na kugeuka rangi yake. Pilipili katika hali hii hutumiwa zaidi kwenye michuzi, kachumbali na kutiwa kwenye makopo.
Pilipili kali, ambayo mara nyingi ni ndogo ndogo, kwa kawaida huvunwa baada ya kupevuka na kuwa nyekundu. Halafu hutumiwa katika mapishi na vyakula mbali mbali, lakini sehemu kubwa zaidi hukaushwa na kusagwa ili kupata unga wake.

Magonjwa
Damping- off, Bacteria Spot, Fusarium wilt na Antracnose, ni miongoni mwa magonjwa yashambuliayo zao hili. Tuseme magonjwa ya pilipili ni sawa na ya Nyanya. Hivyo njia za kupigana nayo ni sawa.
Wadudu: Wadudu ambao hushambulia zao hi wengi, lakini walio wabaya zaidi ni Aphids, Cut worm, Flea beetle, Pepper weevil na Pepper Maggot.
Kinga: Parathion 1% au Chlrdane 5%. Dawa itumiwe mara wadudu watokeapo na kurudiwa kila baada ya siku 7.

Comments

Popular posts from this blog

Kanuni za Ufugaji Bora wa Mbuzi na Kondoo

Utangulizi Mbuzi na kondoo wanaweza kufugwa kwa gharama nafuu na kuishi katika mazingira magumu kama ya maradhi na ukame ikilinganishwa na ng’ombe. Kutokana na umbile lao dogo wanaweza kufugwa katika eneo dogo na pia wanaweza kuhudumiwa na familia yenye nguvukazi na kipato kidogo. Uzao wa muda mfupi unamwezesha mfugaji kupata mbuzi/kondoo wengi kwa kipindi kifupi. Wanyama hao hufugwa kwa ajili ya nyama, maziwa, ngozi, sufu na mazao mengine kwa matumizi ya familia na kuongeza kipato.  Kanuni za kuzingatia Ufugaji bora wa mbuzi na kondoo uzingatie kanuni zifuatazo:- Wafugwe kwenye banda au zizi bora, Wachaguliwe kutokana na sifa za koo/aina na lengo la uzalishaji (nyama, maziwa au sufu), Wapatiwe lishe sahihi kulingana na umri na mahitaji ya mwili, Kuzingatia mbinu za kudhibiti magonjwa kama inavyoshauriwa na mtaalam wa mifugo, Kuweka na kutunza kumbukumbu sahihi za uzalishaji; na  Kuzalisha nyama, maziwa au sufu yenye ubora unaokidhi mahitaji ya soko Zizi au Banda la Mbuzi/Kond...

Kilimo Bora cha Alizeti - Uzalishaji, Uangalizi, Uvunaji na Uhifadhi

Utangulizi Alizeti hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Shinyanga, Singida, Dodoma, Iringa, Tabora, Morogoro, Ruvuma, Mbeya, Arusha, Manyara, na RukwaZao hili hulimwa kwa ajili ya chakula na biashara. Mambo muhimu ya kuzingatia wakati wa uzalishaji Kuchagua aina bora ya mbegu Chagua aina bora ya mbegu inayovumilia magonjwa, wadudu, inayotoa mazao mengi na kiwango kikubwa cha mafuta. Vilevile chagua aina ya mbegu ambayo hukomaa kwa wakati mmoja ili kurahisisha uvunaji. Kuweka mbolea Rutubisha udongo kwa kutumia mbolea za mboji na samadi ili kupata mazao mengi na bora. Kudhibiti wadudu na magonjwa Alizeti hushambuliwa na magonjwa ya majani, mizizi na masuke ambayo husababisha upungufu wa mavunoHivyo ni muhimu kuyadhibiti ili kupata mavuno mengi na boraPia ndege hupunguza mavuno kwa kiasi cha asilimia 50 au zaidiNjia ya kudhibiti ndege ni kwa kuwafukuza na kupanda mbegu zinazokomaa mapema. Maandalizi kabla ya kuvuna;  Ukaguzi  Kagua shamba kuona kama alizeti imekomaaAlizeti hukomaa ...

Utengenezaji wa Chakula cha Kuku wa Nyama (Bloilers)

Utangulizi Kuku wa nyama wana mahitaji yafuatayo ya viinilishe katika chakula ili wakue vizuri Viinilisha vya wanga 60-65%   Protini 30-35%   Madini 2-8% Chakula cha Vifaranga Chakula hiki hutengenezwa katika namna ya kumsaidia kifaranga aweze kumeza vizuri na hivyo hakitakiwi kuwa katika punje punje. Hata kama utanunua pumba, ni vema kuzipitisha kwenye mashine ili ziwe laini zaidi.  Mahitaji (kgs)  Unga wa dona wa nafaka kama mahindi au mtama 40  Pumba za mtama au mahindi au uwele 27  Mashudu ya alizeti au ufuta, au pamba au karanga n.k. 20  Unga wa mifupa au chokaa ya kuku (DCP) 2.25  Dagaa au mabaki ya samaki (sangara fish meal) 10  Chumvi ya jikoni 0.5  Virutubisho (Broiler premix) 0.25  Jumla utapata 100Kg. Chakula cha kukuzia – growers mash Mahitaji (Kg) Mahindi yaliyobarazwa au mtama au uwele 25   Pumba za mtama au mahindi au uwele 44   Mashudu ya alizeti au ufuta, au pamba au karanga n.k. 17   Unga wa mifupa a...