Skip to main content

Kilimo Bora cha Viazi Mviringo


Utangulizi
Viazi mviringo ni moja ya mazao muhimu katika mazao ya mizizi ambalo huzalishwa kwa wingi katika mikoa ya Mbeya, Iringa, Rukwa, Kilimanjaro, Arusha, Mara na Tanga. Uzalishaji wake ni wastani wa tani 340,000 kwa mwaka. Zao hili huchangia kwa kiasi kikubwa katika uchumi wa mkulima kama zao la biashara na chakula.
Mambo Muhimu ya Uzalishaji
Ubora wa zao la viazi mviringo hutegemea sana matunzo ya zao hilo wakati wa uzalishaji. Viazi vinavyopata matunzo mazuri hutoa mazao yenye ubora unaotakiwa katika hifadhi ya muda mrefu na usindikaji. Hivyo wakati wa uzalishaji ni muhimu kuzingatia yafuatayo:

Kuchagua  mbegu
Chagua aina ya mbegu kufuatana na mahitaji ya soko na nayovumilia mashambulizi ya magonjwa. Tumia mbegu bora isiyo na magonjwa na inayozaa mazao mengi na bora.
Kuweka mbolea
  • Viazi vinahitaji rutuba ya kutosha ili kutoa mazao mengi na bora.
  • Tumia mbolea za asili ili kudumisha rutuba.
  •  Utayarishaji, Hifadhi na Usindikaji wa Mazao ya Mizizi baada ya Kuvuna
  •  Iwapo ni lazima kutumia mbolea za viwandani ni muhimu kupata ushauri wa
  • kitaalam kuhusu aina na viwango vya mbolea.
Kupalilia
  • Palilia ili kuondoa magugu na kuruhusu mimea kutumia unyevu na rutuba vizuri.
  • Wakati wa palizi pandishia udongo kwenye mimea ili kuepusha jua linaloweza kushusha ubora wa zao. Viazi vilivyopigwa na jua hubadilika rangi na kuwa vya kijani na ubora hushuka. Viazi vya namna hii huwa havihifadhiki kwa muda mrefu.
Kupanda kwa nafasi
  • Ni muhimu kuzingatia nafasi ya kupanda ili kupata mazao mengi na bora.
  • Panda kwa nafasi kama inavyoshauriwa na wataalamu.
Kudhibiti magonjwa
Zao la viazi mviringo huathirika kwa urahisi na magonjwa ya ukungu, bakteria na virusi ambavyo visipodhibitiwa huweza kuleta hasara kubwa kuanzia shambani hadi ghalani. Hivyo muhimu kukagua shamba ili kubaini na kudhibiti magonjwa kabla ya kusababisha upotevu wa zao.
Maandalizi kabla ya kuvuna
Ni muhimu kufanya maandalizi ya kutosha ili kupunguza upotevu wa mazao.
Kukagua shamba
Kagua shamba kuona kama viazi vimekomaa. Viazi mviringo hukomaa kati ya miezi mitatu hadi minne toka kupanda.
Dalili za viazi mviringo vilivyokomaa
  • Udongo uliozunguka shina hupasuka
  • Majani hubadilika rangi kutoka kijani kuwa ya manjano.
  • Mizizi midogo midogo ya viazi hunyauka.
  • Sehemu ya juu ya mmea hunyauka.
Kuandaa vifaa vya kuvunia na usafiri
Vifaa vya kuvunia
  •  Majembe
  •  Magunia
  •  Vikapu
Usafiri
  •  Magari
  •  Matela ya matrekta
  •  Mikokoteni
Vifungashio
  •  Magunia
Kuvuna
  • Viazi mviringo huweza kuvunwa kwa kutumia jembe la mkono na jembe maalum la kukokotwa na wanyama. Ni muhimu kuvuna wakati kuna unyevu kiasi kwenye udongo ili kurahisisha uvunaji.
  • Kuvuna kwa kutumia mikono
    Mashina ya viazi mviringo yanaweza kung’olewa kwa mkono au kuchimbuliwa kwa jembe kutegemea hali ya udongo.
  • Uangalifu ni muhimu ili kuepuka kukata au kuchubua viazi.
    Ng’oa viazi na kung’uta udongo
    Viache shambani kwa muda wa siku moja ili vinyauke na kuimarisha ngozi. (curing)
  • Weka kwenye magunia au kwenye vikapu na vipeleke sehemu ya kusafishia, kuchambulia na kufungashia

Comments

Popular posts from this blog

Utengenezaji wa Chakula cha Kuku wa Nyama (Bloilers)

Utangulizi Kuku wa nyama wana mahitaji yafuatayo ya viinilishe katika chakula ili wakue vizuri Viinilisha vya wanga 60-65%   Protini 30-35%   Madini 2-8% Chakula cha Vifaranga Chakula hiki hutengenezwa katika namna ya kumsaidia kifaranga aweze kumeza vizuri na hivyo hakitakiwi kuwa katika punje punje. Hata kama utanunua pumba, ni vema kuzipitisha kwenye mashine ili ziwe laini zaidi.  Mahitaji (kgs)  Unga wa dona wa nafaka kama mahindi au mtama 40  Pumba za mtama au mahindi au uwele 27  Mashudu ya alizeti au ufuta, au pamba au karanga n.k. 20  Unga wa mifupa au chokaa ya kuku (DCP) 2.25  Dagaa au mabaki ya samaki (sangara fish meal) 10  Chumvi ya jikoni 0.5  Virutubisho (Broiler premix) 0.25  Jumla utapata 100Kg. Chakula cha kukuzia – growers mash Mahitaji (Kg) Mahindi yaliyobarazwa au mtama au uwele 25   Pumba za mtama au mahindi au uwele 44   Mashudu ya alizeti au ufuta, au pamba au karanga n.k. 17   Unga wa mifupa au chokaa ya kuku (DCP) 3.25   Dagaa au mabaki ya samaki (fish meal) 1

Aina Za Miti ya Minazi

AINA ZA MINAZI Inafaa mkulima kufahamu kuna aina mbali mbali za minazi na ina mahitaji tofauti katika ukuaji. Ujuzi huu utamsaidia katika kuchagua aina ya minazi itakayofaa kwa eneo lake na kwa kiwango chake cha utunzaji. KUNA AINA TATU ZA MINAZI Minazi mirefu ya asili Minazi mifupi Minazi chotara MINAZI MIREFU YA ASILI (EAT) Minazi ya aina hii ndiyo inayojulikana na wakulima wengi kwa vile ni ya kiasili na imezoea mazingira yetu. Minazi hii huchukua miaka 6-8 tangu kupandikizwa hadi kuzaa. Minazi ya aina hii huvumilia ukame na inao uwezo wa kutoa wastani wa nazi 40 kwa mwaka. Nazi huwa kubwa na zenye nyama nene ambayo inafaa kwa kupikia na kukamua mafuta. Minazi hii huishi kad ya miaka 60 na kuendelea. Nchini Tanzania, minazi hii hustawi vyema ukanda wa pwani sehemu zisizo na mawe na ambazo hazituamishi maji. MINAZI MIFUPI (DWARF) Minazi ya aina hii huzaa mapema kuanzia miaka miwili. Huzaa nazi nyingi na ndogo. Nazi hizi huwa na nyama nyembamba hivyo hutumika kwa nnadafu. Minazi huhit

Kilimo cha Miti ya Mbao - Uwekezaji wa Muda wa Kati na Mrefu

Utangulizi Kilimo cha miti ni uwekezaji wa muda wa kati na mrefu (mid & long term investments). Ila kwa kawaida jamii nyingi hasa za kiafrika huwa hazivutiwi na uwekezaji wa muda mrefu. Hata hivyo kama una mpango wa kuwa imara kiuchumi inashauriwaau yakupasa kufikiria na kujifunza aina za uwekezaji wa muda mrefu. Miti hutumika kwa matumizi mengi mfano mbao, nguzo za umeme na kujengea, mapambo, kuni na mkaa, kuzalisha matunda, mitishamba na madawa,  utengenezeaji wa karatasi n.k.  Mchanganuo Ekari moja ya shamba unaweza kupanda miti mia sita (500) mpaka mia saba (700). Gharama za kununua mashamba au maeneo ya kupandia miti hutegemea na eneo. Kwa  sehemu nyingi za vijijini maeneo kwa ekari moja hayazidi laki 5.  Miche ya kununua mfano Mitiki huuzwa kuanzia elfu moja (1000) kwa mche mmoja Gharama ya kununua miche =  1000 * 600 = 600,000   Pia unaweza kuokoa gharama za kununua miche kwa kuioteshe mwenyewe ktk vitalu na kuiamishia shambani baada ya kustawi vizuri na kuwa imara.  Mf. Mbe