Skip to main content

Kilimo Bora cha Viazi Mviringo


Utangulizi
Viazi mviringo ni moja ya mazao muhimu katika mazao ya mizizi ambalo huzalishwa kwa wingi katika mikoa ya Mbeya, Iringa, Rukwa, Kilimanjaro, Arusha, Mara na Tanga. Uzalishaji wake ni wastani wa tani 340,000 kwa mwaka. Zao hili huchangia kwa kiasi kikubwa katika uchumi wa mkulima kama zao la biashara na chakula.
Mambo Muhimu ya Uzalishaji
Ubora wa zao la viazi mviringo hutegemea sana matunzo ya zao hilo wakati wa uzalishaji. Viazi vinavyopata matunzo mazuri hutoa mazao yenye ubora unaotakiwa katika hifadhi ya muda mrefu na usindikaji. Hivyo wakati wa uzalishaji ni muhimu kuzingatia yafuatayo:

Kuchagua  mbegu
Chagua aina ya mbegu kufuatana na mahitaji ya soko na nayovumilia mashambulizi ya magonjwa. Tumia mbegu bora isiyo na magonjwa na inayozaa mazao mengi na bora.
Kuweka mbolea
  • Viazi vinahitaji rutuba ya kutosha ili kutoa mazao mengi na bora.
  • Tumia mbolea za asili ili kudumisha rutuba.
  •  Utayarishaji, Hifadhi na Usindikaji wa Mazao ya Mizizi baada ya Kuvuna
  •  Iwapo ni lazima kutumia mbolea za viwandani ni muhimu kupata ushauri wa
  • kitaalam kuhusu aina na viwango vya mbolea.
Kupalilia
  • Palilia ili kuondoa magugu na kuruhusu mimea kutumia unyevu na rutuba vizuri.
  • Wakati wa palizi pandishia udongo kwenye mimea ili kuepusha jua linaloweza kushusha ubora wa zao. Viazi vilivyopigwa na jua hubadilika rangi na kuwa vya kijani na ubora hushuka. Viazi vya namna hii huwa havihifadhiki kwa muda mrefu.
Kupanda kwa nafasi
  • Ni muhimu kuzingatia nafasi ya kupanda ili kupata mazao mengi na bora.
  • Panda kwa nafasi kama inavyoshauriwa na wataalamu.
Kudhibiti magonjwa
Zao la viazi mviringo huathirika kwa urahisi na magonjwa ya ukungu, bakteria na virusi ambavyo visipodhibitiwa huweza kuleta hasara kubwa kuanzia shambani hadi ghalani. Hivyo muhimu kukagua shamba ili kubaini na kudhibiti magonjwa kabla ya kusababisha upotevu wa zao.
Maandalizi kabla ya kuvuna
Ni muhimu kufanya maandalizi ya kutosha ili kupunguza upotevu wa mazao.
Kukagua shamba
Kagua shamba kuona kama viazi vimekomaa. Viazi mviringo hukomaa kati ya miezi mitatu hadi minne toka kupanda.
Dalili za viazi mviringo vilivyokomaa
  • Udongo uliozunguka shina hupasuka
  • Majani hubadilika rangi kutoka kijani kuwa ya manjano.
  • Mizizi midogo midogo ya viazi hunyauka.
  • Sehemu ya juu ya mmea hunyauka.
Kuandaa vifaa vya kuvunia na usafiri
Vifaa vya kuvunia
  •  Majembe
  •  Magunia
  •  Vikapu
Usafiri
  •  Magari
  •  Matela ya matrekta
  •  Mikokoteni
Vifungashio
  •  Magunia
Kuvuna
  • Viazi mviringo huweza kuvunwa kwa kutumia jembe la mkono na jembe maalum la kukokotwa na wanyama. Ni muhimu kuvuna wakati kuna unyevu kiasi kwenye udongo ili kurahisisha uvunaji.
  • Kuvuna kwa kutumia mikono
    Mashina ya viazi mviringo yanaweza kung’olewa kwa mkono au kuchimbuliwa kwa jembe kutegemea hali ya udongo.
  • Uangalifu ni muhimu ili kuepuka kukata au kuchubua viazi.
    Ng’oa viazi na kung’uta udongo
    Viache shambani kwa muda wa siku moja ili vinyauke na kuimarisha ngozi. (curing)
  • Weka kwenye magunia au kwenye vikapu na vipeleke sehemu ya kusafishia, kuchambulia na kufungashia

Comments

Popular posts from this blog

Uandaaji na Uoteshaji wa Mbegu za Mitiki

Utangulizi Mbegu za mitiki zinapatikana Tanzania Tree Seed Agency wako Msamvu Morogoro.Kilo moja ya mbegu za mitiki inatosha kuotesha kwenye shamba la hekta moja, ambayo ni wastani wa miti 1500 Matayarisho: Ganda la nje la mbengu ya mtiki ni gumu sana na lina sumu mbaya.Unatakiwa uloweke mbegu ya mitiki kwa masaa 72, na kila baada ya masaa 12 unatakiwa ubadilishe maji kwa kumwaga maji ya zamani na kuweka maji mapya. Baada ya masaa 72 anika mbegu zako juani kwa masaa 12 (zianikike ktk bati). Tengeneza kitalu, weka mbolea ya wanyama au mboji, kisha panda mbegu zako kwenye kitalu. Mwangilia maji kila siku asubuhi na jioni, mbegu zitaanza kuota baada ya siku 10 hadi 20. Miche ikifikia urefu wa futi moja, unaweza sasa kuiotesha kwenye shamba lako ulilotayarisha kwa ajili ya kuotesha miti. Kabla ya kung’'oa miche hakikisha unamwaga maji mengi, ili mizizi isikatike sana, kisha chukua kisu chenye makali ya kutosha na kata ncha ya juu ya mti na ondoa majani, hii inasaidia mti kuchipuka upya...

Kanuni za Ufugaji Bora wa Mbuzi na Kondoo

Utangulizi Mbuzi na kondoo wanaweza kufugwa kwa gharama nafuu na kuishi katika mazingira magumu kama ya maradhi na ukame ikilinganishwa na ng’ombe. Kutokana na umbile lao dogo wanaweza kufugwa katika eneo dogo na pia wanaweza kuhudumiwa na familia yenye nguvukazi na kipato kidogo. Uzao wa muda mfupi unamwezesha mfugaji kupata mbuzi/kondoo wengi kwa kipindi kifupi. Wanyama hao hufugwa kwa ajili ya nyama, maziwa, ngozi, sufu na mazao mengine kwa matumizi ya familia na kuongeza kipato.  Kanuni za kuzingatia Ufugaji bora wa mbuzi na kondoo uzingatie kanuni zifuatazo:- Wafugwe kwenye banda au zizi bora, Wachaguliwe kutokana na sifa za koo/aina na lengo la uzalishaji (nyama, maziwa au sufu), Wapatiwe lishe sahihi kulingana na umri na mahitaji ya mwili, Kuzingatia mbinu za kudhibiti magonjwa kama inavyoshauriwa na mtaalam wa mifugo, Kuweka na kutunza kumbukumbu sahihi za uzalishaji; na  Kuzalisha nyama, maziwa au sufu yenye ubora unaokidhi mahitaji ya soko Zizi au Banda la Mbuzi/Kond...

Utengenezaji wa Chakula cha Kuku wa Nyama (Bloilers)

Utangulizi Kuku wa nyama wana mahitaji yafuatayo ya viinilishe katika chakula ili wakue vizuri Viinilisha vya wanga 60-65%   Protini 30-35%   Madini 2-8% Chakula cha Vifaranga Chakula hiki hutengenezwa katika namna ya kumsaidia kifaranga aweze kumeza vizuri na hivyo hakitakiwi kuwa katika punje punje. Hata kama utanunua pumba, ni vema kuzipitisha kwenye mashine ili ziwe laini zaidi.  Mahitaji (kgs)  Unga wa dona wa nafaka kama mahindi au mtama 40  Pumba za mtama au mahindi au uwele 27  Mashudu ya alizeti au ufuta, au pamba au karanga n.k. 20  Unga wa mifupa au chokaa ya kuku (DCP) 2.25  Dagaa au mabaki ya samaki (sangara fish meal) 10  Chumvi ya jikoni 0.5  Virutubisho (Broiler premix) 0.25  Jumla utapata 100Kg. Chakula cha kukuzia – growers mash Mahitaji (Kg) Mahindi yaliyobarazwa au mtama au uwele 25   Pumba za mtama au mahindi au uwele 44   Mashudu ya alizeti au ufuta, au pamba au karanga n.k. 17   Unga wa mifupa a...