Skip to main content

Magonjwa ya Kuku - Chanjo, Kinga na Matibabu




Utangulizi
Tunashauri jamii kufuga kuku wa kuchanganya damu (cross breed) yaani pandisha kuku wa kienyeji na wale wa kisasa (indigenous + Pure breeds) ili kuweza kupata kuku ambao kwa kiasi fulani huhimili magonjwa. Wafugaji wengi wanakosea sana taratibu za kuwalisha kuku kitu ambacho kinawapa hasara lakini kama akiwa ni mtu wa kuzingatia anaepukana na magonjwa yanayoweza kujitokeza kutokana na uzembe wake. Chakula nacho ni tatizo watu wengi wanakosea vipimo, kuku anayetaga anatakiwa ale kwa kiwango maalum kinachotakiwa.kuku akila na kupitiliza kiwango au kupunguza hatagi kwa kiwango kinachotakiwa au asitage sana itategemea ameathirika kwa kiwango gani kwa sababu akiwa na mafuta kwa wingi hatagi,akipungukiwa na chakula hatagi.
Minyoo na utitiri nalo ni tatizo linachangia kuku kutokutaga, unashauriwa kumpa kuku dawa za minyoo na utitiri kwa wakati. Inashauriwa kutumia mabanda ya ghorofa kwa ajili ya vifaranga ili kuepukana na bacteria wanatokana maranda kwetu utajionea na ni faida kwako.

Magonjwa yanayosababishwa na virusi
  1. Mdondo (Newcastle):
    Dalili zake:
    kuku kukohoa,kuhema kwa shida,kutokwa na ute mdomoni na puani,hupatwa na kizunguzungu, kuharrisha mharo wa kijani na manjano na hatimaye kuku hufa ghafla. Vifo huweza kufikia asilimia90
  2. Ndui ya kuku: fowlpox)
    Kuku hupatwa na vipele vya mviringo kwenye upanga, (masikio,miguu na sehemu zisizo na manyoya.vifo vichache kwa kuku wakubwa, wadogo huweza kufa nusu ya kundi.CHANJO WIKI YA NANE (wapewe antibiotic na vitamini) hakuna tiba)
  3. Mahepe (.marek’s disease)Kuku kupooza miguu, mabawa na shingo huweza kupinda, mara nyingi huwapata kuku wenye umri wa wiki ya 16 hadi 30.kiasi cha robo ya mitemba wanaweza kufa. (chanja vifaranga wakiwa na umri wa siku moja)
  4. Gumboro :vifaranga huharisha mharo mweupe,huhangaikahangaika, hushindwa kuhema, manyoya husimama, hudumaa, hutetemeka na hatimaye hufa.vifo vyaweza kufikia 5% hadi 10%. (Hakuna tiba wapatiwe chanjo ya gumburo)
  5. Magonjwa yashambuliayo mfumo wa hewa
    (Infectious bronchitis, laryngotracheitis or chicken influenza) 
    upungufu wa mayai kwa kuku wanaotaga,vifaranga hupata matatizo ya kupumua na kupiga chafya na hufa kwa wingi
     
    (huzuiwa kwa chanjo, hakuna tiba.)
  6. Mafua makali ya ndege:
    kupumua kwa shida, kukohoa na kupiga chafya, sehemu za kikole(kidevu na kishungi) hubadilika na kuwa rangi ya zambarau,kutokwa na machozi,kupinda shingo na kuanza kuzunguka, kuvimba kichwa, kuharisha kinyesi chenye majimaji, rangi ya kijani na baadaye kinyesi cheupe.
    (hakuna tiba muone daktari)
  7. Homa ya matumbo: (salmonella gallinarum)
    ugonjwa huu unaweza kurithiwa kupitia kwenye mayai au kuambukizwa kutokana na kuku wagonjwa, kinyesi, kudonoana, na mazingira machafu, 
    Kuku huharisha mharo wa kijani, vilemba na upanga hupauka kutokana na upungufu wa damu, manyoya husimama.vifo huweza kufikia 50%. Weka banda katika hali ya usafi,ondoa kuku waliougua,usitumie mayai yenye ugonjwa kuangulia.
  8. Pullorum bacillary white diarrhea (bacteria salmonella pullorum)huathiri zaidi vifaranga(kabla ya umri wa wiki 4) vifaranga hujikusanya pamoja na kutetemeka kama waliopatwa na baridi.huharisha mharo mweupe hamu ya kula hupungua,manyoa hunyea na hupumua kwa taabu.vifo huweza kufikia asilimia 50.
  9. Kipindupindu cha kuku(Fowl cholera)
    kuku kuhara mharo wa rangi ya njano.husinzia na kulegea,hulala kichwa kikining’inia kwenye mabawa.manyoya husimama,kuhema kwa shida,hushindwa kusimama na hatimaye hufa.vifo huweza kufikia asilimia 50 
    Usafi wa banda
    (huweza kutibika kwa dawa ya sulfa)
  10. Ugonjwa unaoshambulia mfumo wa hewa (chronic respiratory)
    Kuku kupata mafua, kukohoa kushindwa kupumua, kutokwa na makamasi,vifaranga hudumaa,utagaji hupungua na viungo vya mifupa huweza kuvimba
    Tiba: antibiotic hutibu,usafi wa banda.
  11. Ugonjwa wa kuhara damu:
    Kuku huharisha kinyesi kilichochanganyika na damu na mara nyingine damu tupu,hudhoofisha kuku, huteremsha mabawa na hatimaye kuku huweza kufa. 
    Usafi wa banda,hutibiwa kwa kutumia dawa kama vile Amprolium.salfa na Esb3.Muone daktar.i
[Imetolewa na TAVEPA]

Comments

Popular posts from this blog

Kanuni za Ufugaji Bora wa Mbuzi na Kondoo

Utangulizi Mbuzi na kondoo wanaweza kufugwa kwa gharama nafuu na kuishi katika mazingira magumu kama ya maradhi na ukame ikilinganishwa na ng’ombe. Kutokana na umbile lao dogo wanaweza kufugwa katika eneo dogo na pia wanaweza kuhudumiwa na familia yenye nguvukazi na kipato kidogo. Uzao wa muda mfupi unamwezesha mfugaji kupata mbuzi/kondoo wengi kwa kipindi kifupi. Wanyama hao hufugwa kwa ajili ya nyama, maziwa, ngozi, sufu na mazao mengine kwa matumizi ya familia na kuongeza kipato.  Kanuni za kuzingatia Ufugaji bora wa mbuzi na kondoo uzingatie kanuni zifuatazo:- Wafugwe kwenye banda au zizi bora, Wachaguliwe kutokana na sifa za koo/aina na lengo la uzalishaji (nyama, maziwa au sufu), Wapatiwe lishe sahihi kulingana na umri na mahitaji ya mwili, Kuzingatia mbinu za kudhibiti magonjwa kama inavyoshauriwa na mtaalam wa mifugo, Kuweka na kutunza kumbukumbu sahihi za uzalishaji; na  Kuzalisha nyama, maziwa au sufu yenye ubora unaokidhi mahitaji ya soko Zizi au Banda la Mbuzi/Kond...

Kilimo Bora cha Alizeti - Uzalishaji, Uangalizi, Uvunaji na Uhifadhi

Utangulizi Alizeti hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Shinyanga, Singida, Dodoma, Iringa, Tabora, Morogoro, Ruvuma, Mbeya, Arusha, Manyara, na RukwaZao hili hulimwa kwa ajili ya chakula na biashara. Mambo muhimu ya kuzingatia wakati wa uzalishaji Kuchagua aina bora ya mbegu Chagua aina bora ya mbegu inayovumilia magonjwa, wadudu, inayotoa mazao mengi na kiwango kikubwa cha mafuta. Vilevile chagua aina ya mbegu ambayo hukomaa kwa wakati mmoja ili kurahisisha uvunaji. Kuweka mbolea Rutubisha udongo kwa kutumia mbolea za mboji na samadi ili kupata mazao mengi na bora. Kudhibiti wadudu na magonjwa Alizeti hushambuliwa na magonjwa ya majani, mizizi na masuke ambayo husababisha upungufu wa mavunoHivyo ni muhimu kuyadhibiti ili kupata mavuno mengi na boraPia ndege hupunguza mavuno kwa kiasi cha asilimia 50 au zaidiNjia ya kudhibiti ndege ni kwa kuwafukuza na kupanda mbegu zinazokomaa mapema. Maandalizi kabla ya kuvuna;  Ukaguzi  Kagua shamba kuona kama alizeti imekomaaAlizeti hukomaa ...

Utengenezaji wa Chakula cha Kuku wa Nyama (Bloilers)

Utangulizi Kuku wa nyama wana mahitaji yafuatayo ya viinilishe katika chakula ili wakue vizuri Viinilisha vya wanga 60-65%   Protini 30-35%   Madini 2-8% Chakula cha Vifaranga Chakula hiki hutengenezwa katika namna ya kumsaidia kifaranga aweze kumeza vizuri na hivyo hakitakiwi kuwa katika punje punje. Hata kama utanunua pumba, ni vema kuzipitisha kwenye mashine ili ziwe laini zaidi.  Mahitaji (kgs)  Unga wa dona wa nafaka kama mahindi au mtama 40  Pumba za mtama au mahindi au uwele 27  Mashudu ya alizeti au ufuta, au pamba au karanga n.k. 20  Unga wa mifupa au chokaa ya kuku (DCP) 2.25  Dagaa au mabaki ya samaki (sangara fish meal) 10  Chumvi ya jikoni 0.5  Virutubisho (Broiler premix) 0.25  Jumla utapata 100Kg. Chakula cha kukuzia – growers mash Mahitaji (Kg) Mahindi yaliyobarazwa au mtama au uwele 25   Pumba za mtama au mahindi au uwele 44   Mashudu ya alizeti au ufuta, au pamba au karanga n.k. 17   Unga wa mifupa a...