Skip to main content

Aina Za Miti ya Minazi


AINA ZA MINAZI
Inafaa mkulima kufahamu kuna aina mbali mbali za minazi na ina mahitaji tofauti katika ukuaji. Ujuzi huu utamsaidia katika kuchagua aina ya minazi itakayofaa kwa eneo lake na kwa kiwango chake cha utunzaji.

KUNA AINA TATU ZA MINAZI
  • Minazi mirefu ya asili
  • Minazi mifupi
  • Minazi chotara
MINAZI MIREFU YA ASILI (EAT)
Minazi ya aina hii ndiyo inayojulikana na wakulima wengi kwa vile ni ya kiasili na imezoea mazingira yetu. Minazi hii huchukua miaka 6-8 tangu kupandikizwa hadi kuzaa. Minazi ya aina hii huvumilia ukame na inao uwezo wa kutoa wastani wa nazi 40 kwa mwaka. Nazi huwa kubwa na zenye nyama nene ambayo inafaa kwa kupikia na kukamua mafuta. Minazi hii huishi kad ya miaka 60 na kuendelea. Nchini Tanzania, minazi hii hustawi vyema ukanda wa pwani sehemu zisizo na mawe na ambazo hazituamishi maji.

MINAZI MIFUPI (DWARF)
Minazi ya aina hii huzaa mapema kuanzia miaka miwili. Huzaa nazi nyingi na ndogo. Nazi hizi huwa na nyama nyembamba hivyo hutumika kwa nnadafu. Minazi huhitaji mvua nyingi na huduma zaidi, kwa sababu hii minazi hupandwa kama mapambo karibu na nyumba. Kwa kawaida minazi hii huishi kati ya miaka 40-50.

MINAZI CHOTARA (HYBRID)
Minazi chotara hutokana na mchanganyiko wa minazi mifupi na mirefu, hivyo ina sifa za minazi aina zote mbili, Sifa hizo ni:
Kukua haraka na huanza kuzaa kati ya miaka 4-5. Kwa kawaida mnazi huzaa zaidi ya nazi 60 kwa mwaka. Nazi huwa kubwa zenye nyama nene hivyo hutumika kwa kupikia na kukamua mafuta. Minazi hii huishi kati ya miaka 60 na kuendelea. Inahitaji udongo ulio na rutuba na uangalizi wa hali yajuu. Minazi hii inashauriwa kupandwa sehemu zenye udongo tifutifu na zinazo pata mvua za kutosha tu kama baadhi ya sehemu za visiwa, mkoa wa Tanga, Pwani na kwenye mabonde ya mikoa ya Kusini.
Taswira
Mpaka sasa kuna aina mbili za chotara ambazo ni MAWA na CAMWA ambazo ubora wake umethibitishwa. Mbegu aina hizi hupatikana katika mashamba ya mbegu yaliopo Zanzibar ambayo yanamilikiwa na Mradi wa Taifa wa Uendelezaji Minazi.


Comments

  1. Nahitaji kufahamu ya kuwa hekari moja inachukua miche mingapi ya minazi

    ReplyDelete
  2. Asante kwa elimu nzuri ila naomba unifahamishe kuwa ekari moja ya shamba la minazi linalotunzwa vizuri linatoa tani ngapi za minazi?

    ReplyDelete
  3. VP mkoa wa arusha unafaaa kwa kilimo cha Nazi?

    ReplyDelete
  4. Je kwa mkoa wetu wa dar es salaam nazi hizi huweza kulimwa sehem za miinuko??

    ReplyDelete
  5. Swali langu ni kwamba Kilimanjaro unaweza ukapanda miti ya minazi na ikazaa vizuriii...??

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

How to Save Watermelon Seeds for Planting on Small Garden

Watermelon seeds from this year's garden can be planted next year. Seeds saved from the fruits of your garden's non-hybrid watermelon plants (Citrullus lanatus) can grow into new plants the following season. Different varieties of watermelons can cross-pollinate, which results in seedlings that aren't exactly like their parent plants. So grow only one watermelon variety in the garden if you want to save the seeds. The large seeds separate from the fruits easily, but they require some preparation to store well. Properly saved watermelon seeds can remain viable up to four years. Cut open a ripe watermelon. Scoop the seeds from the melon's flesh, and place them in a strainer. Rinse the seeds with warm tap water, removing most of the pulp. Add one drop of liquid dish soap, and wash the seeds gently to remove the remaining watermelon juice. Rinse the seeds thoroughly with only water. Spread the seeds on a sheet of wax paper. Dry the seeds for one week, turning them once each...

Kilimo Bora cha Alizeti - Uzalishaji, Uangalizi, Uvunaji na Uhifadhi

Utangulizi Alizeti hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Shinyanga, Singida, Dodoma, Iringa, Tabora, Morogoro, Ruvuma, Mbeya, Arusha, Manyara, na RukwaZao hili hulimwa kwa ajili ya chakula na biashara. Mambo muhimu ya kuzingatia wakati wa uzalishaji Kuchagua aina bora ya mbegu Chagua aina bora ya mbegu inayovumilia magonjwa, wadudu, inayotoa mazao mengi na kiwango kikubwa cha mafuta. Vilevile chagua aina ya mbegu ambayo hukomaa kwa wakati mmoja ili kurahisisha uvunaji. Kuweka mbolea Rutubisha udongo kwa kutumia mbolea za mboji na samadi ili kupata mazao mengi na bora. Kudhibiti wadudu na magonjwa Alizeti hushambuliwa na magonjwa ya majani, mizizi na masuke ambayo husababisha upungufu wa mavunoHivyo ni muhimu kuyadhibiti ili kupata mavuno mengi na boraPia ndege hupunguza mavuno kwa kiasi cha asilimia 50 au zaidiNjia ya kudhibiti ndege ni kwa kuwafukuza na kupanda mbegu zinazokomaa mapema. Maandalizi kabla ya kuvuna;  Ukaguzi  Kagua shamba kuona kama alizeti imekomaaAlizeti hukomaa ...

Agriculture in Tanzania

Introduction Agriculture is main part of Tanzania's economy. As of 2016 Tanzania has over 44 million hectares of arable land with only 33% of this amount being cultivated. More than 80% of the poor population live in rural areas and almost all of them are involved in the farming sector Land is a vital asset in ensuring food security and among the main food crops in Tanzania are maize, sorghum, millet, rice, wheat, beans, cassava, potatoes and bananas. Agricultural products also contributes largely to the country's foreign exchange earnings and over 1 billion dollars is earning from cash crop exports. Cash crops include Coffee, Sisal, Cashew nut, Tea, Cotton and Tobacco. At one point in history Tanzania was the largest producer of sisal in the world. The agriculture sector faces various challenges and has been the governments top priority to develop to reduce poverty.Farming efficiently has been a challenge of many farmers and lack of finances and lack of farming education has l...