Skip to main content

Je wajua Vyura, Ndege, na Wadudu Huboresha Shamba


Lakini unaweza kuwamalizaje wadudu waharibifu shambani mwako bila kutumia dawa? Usisahau kwamba zaidi ya kuwaua wadudu waharibifu, dawa hizo huua viumbe muhimu kama vile minyoo na kuvu. Pia, kumbuka kwamba vyura ni muhimu sana katika kilimo. Chura anaweza kula wadudu waharibifu 10,000 kwa muda wa miezi mitatu naye hachagui anachokula. Yeye hula viumbe wanaoharibu mimea kama vile nyenje, wadudu na viwavi wa aina fulani, na konokono.
Ndege pia hula viumbe waharibifu. Kitabu Gardening Without Poisons chasema kwamba ndege aina ya wren alionekana akiwalisha “makinda wake buibui na viwavi 500 alasiri moja katika majira ya kiangazi.” Ukitaka ndege kadhaa aina ya wren au ndege wengine wanaokula wadudu waje shambani mwako basi weka chakula cha ndege na vifaa vya kujenga kiota mahala wanapoweza kuviona. Muda si muda, utaona wakija! Na vipi wadudu? Wadudu wengi wanaoboresha shamba hula wadudu waharibifu. Ukinunua wadudu aina ya ladybug kisha uwaweke shambani mwako, watawamaliza mara moja wadudu aina ya aphid kwani wanapenda kula wadudu hao sana. Mayai ya kivunja-jungu yanaweza pia kununuliwa na kuwekwa shambani. Mayai hayo yakianguliwa, vivunja-jungu watakula wadudu wote walio karibu nao.

Comments

Popular posts from this blog

Utengenezaji wa Chakula cha Kuku wa Nyama (Bloilers)

Utangulizi Kuku wa nyama wana mahitaji yafuatayo ya viinilishe katika chakula ili wakue vizuri Viinilisha vya wanga 60-65%   Protini 30-35%   Madini 2-8% Chakula cha Vifaranga Chakula hiki hutengenezwa katika namna ya kumsaidia kifaranga aweze kumeza vizuri na hivyo hakitakiwi kuwa katika punje punje. Hata kama utanunua pumba, ni vema kuzipitisha kwenye mashine ili ziwe laini zaidi.  Mahitaji (kgs)  Unga wa dona wa nafaka kama mahindi au mtama 40  Pumba za mtama au mahindi au uwele 27  Mashudu ya alizeti au ufuta, au pamba au karanga n.k. 20  Unga wa mifupa au chokaa ya kuku (DCP) 2.25  Dagaa au mabaki ya samaki (sangara fish meal) 10  Chumvi ya jikoni 0.5  Virutubisho (Broiler premix) 0.25  Jumla utapata 100Kg. Chakula cha kukuzia – growers mash Mahitaji (Kg) Mahindi yaliyobarazwa au mtama au uwele 25   Pumba za mtama au mahindi au uwele 44   Mashudu ya alizeti au ufuta, au pamba au karanga n.k. 17   Unga wa mifupa au chokaa ya kuku (DCP) 3.25   Dagaa au mabaki ya samaki (fish meal) 1

Aina na Faida za kufuga Mbuzi

Utangulizi Ufugaji wa mbuzi hapa ni fursa nadra ambayo Watanzania wengi hawajaiona. Ni ufugaji ambao wenyewe kama mfugaji atazingatia kanuni na misingi ya ufugaji Bora, ni rahisi sana mfugaji kujiondoa kutoka kwenye umasikini na kuwa tajiri. Kitu cha msingi na muhimu ni kwamba,mfugaji lazima awe na eneo pamoja na mtaji wa kuanzia. Hawa ni mbuzi bora walioboreshwa, wanapatikana dodoma. Ni matokeo ya cross breed iliyofanyika kati ya mbuzi wa kienyeji wa dodoma na exotic breed.Hivyo wengi wa uzao wao huzaa mapacha. Mbuzi hawa huuzwa tsh elfu 50, wakiwa na umri wa miezi 5. Sehemu ya kufugia Mbuzi wanatakiwa kufugwa shambani. Shamba ambalo mbuzi wanatakiwa wafugwe linapaswa liwe na sehemu ambayo mbuzi wanaweza kwenda kuchungwa na pia kuwe na chanzo cha maji. Mbuzi kitabia hupenda kulala juu hivyo mabanda yao yanapojengwa lazima yainuliwe juu. Mabanda ya mbuzi si ghari,kwani hujengwa simple. Uzaaji Mbuzi kwa mwaka huzaa mara mbili na ukipata ile mbegu ya wanaozaa mapacha faida yake huwa ni k

Aina Za Miti ya Minazi

AINA ZA MINAZI Inafaa mkulima kufahamu kuna aina mbali mbali za minazi na ina mahitaji tofauti katika ukuaji. Ujuzi huu utamsaidia katika kuchagua aina ya minazi itakayofaa kwa eneo lake na kwa kiwango chake cha utunzaji. KUNA AINA TATU ZA MINAZI Minazi mirefu ya asili Minazi mifupi Minazi chotara MINAZI MIREFU YA ASILI (EAT) Minazi ya aina hii ndiyo inayojulikana na wakulima wengi kwa vile ni ya kiasili na imezoea mazingira yetu. Minazi hii huchukua miaka 6-8 tangu kupandikizwa hadi kuzaa. Minazi ya aina hii huvumilia ukame na inao uwezo wa kutoa wastani wa nazi 40 kwa mwaka. Nazi huwa kubwa na zenye nyama nene ambayo inafaa kwa kupikia na kukamua mafuta. Minazi hii huishi kad ya miaka 60 na kuendelea. Nchini Tanzania, minazi hii hustawi vyema ukanda wa pwani sehemu zisizo na mawe na ambazo hazituamishi maji. MINAZI MIFUPI (DWARF) Minazi ya aina hii huzaa mapema kuanzia miaka miwili. Huzaa nazi nyingi na ndogo. Nazi hizi huwa na nyama nyembamba hivyo hutumika kwa nnadafu. Minazi huhit