Skip to main content

Aina Za Miti ya Minazi


AINA ZA MINAZI
Inafaa mkulima kufahamu kuna aina mbali mbali za minazi na ina mahitaji tofauti katika ukuaji. Ujuzi huu utamsaidia katika kuchagua aina ya minazi itakayofaa kwa eneo lake na kwa kiwango chake cha utunzaji.

KUNA AINA TATU ZA MINAZI
  • Minazi mirefu ya asili
  • Minazi mifupi
  • Minazi chotara
MINAZI MIREFU YA ASILI (EAT)
Minazi ya aina hii ndiyo inayojulikana na wakulima wengi kwa vile ni ya kiasili na imezoea mazingira yetu. Minazi hii huchukua miaka 6-8 tangu kupandikizwa hadi kuzaa. Minazi ya aina hii huvumilia ukame na inao uwezo wa kutoa wastani wa nazi 40 kwa mwaka. Nazi huwa kubwa na zenye nyama nene ambayo inafaa kwa kupikia na kukamua mafuta. Minazi hii huishi kad ya miaka 60 na kuendelea. Nchini Tanzania, minazi hii hustawi vyema ukanda wa pwani sehemu zisizo na mawe na ambazo hazituamishi maji.

MINAZI MIFUPI (DWARF)
Minazi ya aina hii huzaa mapema kuanzia miaka miwili. Huzaa nazi nyingi na ndogo. Nazi hizi huwa na nyama nyembamba hivyo hutumika kwa nnadafu. Minazi huhitaji mvua nyingi na huduma zaidi, kwa sababu hii minazi hupandwa kama mapambo karibu na nyumba. Kwa kawaida minazi hii huishi kati ya miaka 40-50.

MINAZI CHOTARA (HYBRID)
Minazi chotara hutokana na mchanganyiko wa minazi mifupi na mirefu, hivyo ina sifa za minazi aina zote mbili, Sifa hizo ni:
Kukua haraka na huanza kuzaa kati ya miaka 4-5. Kwa kawaida mnazi huzaa zaidi ya nazi 60 kwa mwaka. Nazi huwa kubwa zenye nyama nene hivyo hutumika kwa kupikia na kukamua mafuta. Minazi hii huishi kati ya miaka 60 na kuendelea. Inahitaji udongo ulio na rutuba na uangalizi wa hali yajuu. Minazi hii inashauriwa kupandwa sehemu zenye udongo tifutifu na zinazo pata mvua za kutosha tu kama baadhi ya sehemu za visiwa, mkoa wa Tanga, Pwani na kwenye mabonde ya mikoa ya Kusini.
Taswira
Mpaka sasa kuna aina mbili za chotara ambazo ni MAWA na CAMWA ambazo ubora wake umethibitishwa. Mbegu aina hizi hupatikana katika mashamba ya mbegu yaliopo Zanzibar ambayo yanamilikiwa na Mradi wa Taifa wa Uendelezaji Minazi.


Comments

  1. Nahitaji kufahamu ya kuwa hekari moja inachukua miche mingapi ya minazi

    ReplyDelete
  2. Asante kwa elimu nzuri ila naomba unifahamishe kuwa ekari moja ya shamba la minazi linalotunzwa vizuri linatoa tani ngapi za minazi?

    ReplyDelete
  3. VP mkoa wa arusha unafaaa kwa kilimo cha Nazi?

    ReplyDelete
  4. Je kwa mkoa wetu wa dar es salaam nazi hizi huweza kulimwa sehem za miinuko??

    ReplyDelete
  5. Swali langu ni kwamba Kilimanjaro unaweza ukapanda miti ya minazi na ikazaa vizuriii...??

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

Kanuni za Ufugaji Bora wa Mbuzi na Kondoo

Utangulizi Mbuzi na kondoo wanaweza kufugwa kwa gharama nafuu na kuishi katika mazingira magumu kama ya maradhi na ukame ikilinganishwa na ng’ombe. Kutokana na umbile lao dogo wanaweza kufugwa katika eneo dogo na pia wanaweza kuhudumiwa na familia yenye nguvukazi na kipato kidogo. Uzao wa muda mfupi unamwezesha mfugaji kupata mbuzi/kondoo wengi kwa kipindi kifupi. Wanyama hao hufugwa kwa ajili ya nyama, maziwa, ngozi, sufu na mazao mengine kwa matumizi ya familia na kuongeza kipato.  Kanuni za kuzingatia Ufugaji bora wa mbuzi na kondoo uzingatie kanuni zifuatazo:- Wafugwe kwenye banda au zizi bora, Wachaguliwe kutokana na sifa za koo/aina na lengo la uzalishaji (nyama, maziwa au sufu), Wapatiwe lishe sahihi kulingana na umri na mahitaji ya mwili, Kuzingatia mbinu za kudhibiti magonjwa kama inavyoshauriwa na mtaalam wa mifugo, Kuweka na kutunza kumbukumbu sahihi za uzalishaji; na  Kuzalisha nyama, maziwa au sufu yenye ubora unaokidhi mahitaji ya soko Zizi au Banda la Mbuzi/Kond...

Kilimo Bora cha Alizeti - Uzalishaji, Uangalizi, Uvunaji na Uhifadhi

Utangulizi Alizeti hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Shinyanga, Singida, Dodoma, Iringa, Tabora, Morogoro, Ruvuma, Mbeya, Arusha, Manyara, na RukwaZao hili hulimwa kwa ajili ya chakula na biashara. Mambo muhimu ya kuzingatia wakati wa uzalishaji Kuchagua aina bora ya mbegu Chagua aina bora ya mbegu inayovumilia magonjwa, wadudu, inayotoa mazao mengi na kiwango kikubwa cha mafuta. Vilevile chagua aina ya mbegu ambayo hukomaa kwa wakati mmoja ili kurahisisha uvunaji. Kuweka mbolea Rutubisha udongo kwa kutumia mbolea za mboji na samadi ili kupata mazao mengi na bora. Kudhibiti wadudu na magonjwa Alizeti hushambuliwa na magonjwa ya majani, mizizi na masuke ambayo husababisha upungufu wa mavunoHivyo ni muhimu kuyadhibiti ili kupata mavuno mengi na boraPia ndege hupunguza mavuno kwa kiasi cha asilimia 50 au zaidiNjia ya kudhibiti ndege ni kwa kuwafukuza na kupanda mbegu zinazokomaa mapema. Maandalizi kabla ya kuvuna;  Ukaguzi  Kagua shamba kuona kama alizeti imekomaaAlizeti hukomaa ...

Utengenezaji wa Chakula cha Kuku wa Nyama (Bloilers)

Utangulizi Kuku wa nyama wana mahitaji yafuatayo ya viinilishe katika chakula ili wakue vizuri Viinilisha vya wanga 60-65%   Protini 30-35%   Madini 2-8% Chakula cha Vifaranga Chakula hiki hutengenezwa katika namna ya kumsaidia kifaranga aweze kumeza vizuri na hivyo hakitakiwi kuwa katika punje punje. Hata kama utanunua pumba, ni vema kuzipitisha kwenye mashine ili ziwe laini zaidi.  Mahitaji (kgs)  Unga wa dona wa nafaka kama mahindi au mtama 40  Pumba za mtama au mahindi au uwele 27  Mashudu ya alizeti au ufuta, au pamba au karanga n.k. 20  Unga wa mifupa au chokaa ya kuku (DCP) 2.25  Dagaa au mabaki ya samaki (sangara fish meal) 10  Chumvi ya jikoni 0.5  Virutubisho (Broiler premix) 0.25  Jumla utapata 100Kg. Chakula cha kukuzia – growers mash Mahitaji (Kg) Mahindi yaliyobarazwa au mtama au uwele 25   Pumba za mtama au mahindi au uwele 44   Mashudu ya alizeti au ufuta, au pamba au karanga n.k. 17   Unga wa mifupa a...